Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu

WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi Kuu Tanzania, timu hiyo itawakosa wachezaji wake muhimu wanaokabiliwa na majeraha akiwamo mshambuliaji Laurindo Dilson ‘Depu’.

 Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea  mchezo huo utakaopigwa kesho saa 10:00 alasiri, katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha, Kocha Mkuu wa Yanga Pedro Goncalves  amesema wamekuwa na ratiba ngumu ya michezo mfululizo ukizingatia wametoka kucheza mechi ngumu siku chache zilizopita tofauti na wapinzani wao.

Amesema wanakwenda kukabiliana na timu ambayo imepata muda wa kutosha wa mapumziko na maandalizi lakini wamejipanga kuchukua pointi tatu.

“Pia tumekubwa na idadi kubwa ya majeruhi. Lakini hali hiyo inatoa fursa kwa wachezaji wengine wenye hali nzuri,” amesema.

Uongozi wa Klabu ya Yanga umetoa taarifa ya  kuthibitisha kuwa wachezaji wake wanne wakiwemo  Chadrack Boka, Edmund John pamoja na Ibrahim Abdullah ‘Bacca’ wamepata majeraha na wanatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa.

Wachezaji wengine ni Chadrack Boka ambaye amepata jeraha la enka ya mguu wa kushoto na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili, na Edmund John ambaye amepata jeraha la bega na atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki mbili.

spot_img

Latest articles

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

More like this

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...