Isha Mashauzi aibukia Mtata Mtatuzi

Na Winfrida Mtoi

Mwanamuziki wa miondoko ya taarabu, Isha Mashauzi atakuwa miongoni mwa watakaoshudia a pambano la ngumi la bondia Hassan Mwakinyo lililopewa jina la Mtata Mtatuzi.

Mwakinyo anatarajiwa kupanda ulingoni Januari 27, 2024 kuzichapa na Mbiya Kanku raia wa DR Congo pambano la ubingwa wa WBO Afrika litakalopigwa Amani Complex Indoor Arena, Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuelekea visiwani humo, Isha amesema alikuwepo Ubungo Plaza Desemba 26, 2023 na kushudia vitasa hasa kwa wanawake hivyo kuamua kwenda tena Zanzibar kuona burudani hiyo.

Ameeleza kuwa lengo ni kupeana sapoti kwa sababu ngumi na muziki vyote vinakwenda pamoja.

“Ngumi ni muziki na muziki ni ngumi. Zamani tulikuwa tunaamini kwamba wanaopenda michezo hii ni wanaume tu na ni hatari lakini sasa hivj hata watoto wa kike wanafanya vizuri ndiyo maana nikaamua kuja kusapoti,” amesema Isha.

Amesema kwa hali ilivyo Tanzania itafika mbali kupitia mchezo wa ngumi, huku akiwataka mashabiki kununua tiketi ili kushuhudia mapambano hayo.

Kwa upande wake Mwakinyo amesema ameshakamilisha maandalizi na kutamba kuwa yeye ni bondia mkubwa hana mpinzani nchini.

spot_img

Latest articles

Waogeleaji wa Lake Victoria Sports Club waahidi kuing’arisha Tanzania Kimataifa

Na Mwandishi Wetu Jumla ya waogeleaji sita  chipukizi wa Lake Victoria Sports Club  ya jijini...

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...

Kafulila: Hatuwezi kujenga uchumi wa nchi bila kushirikisha sekta binafsi

Na Tatu Mohamed, Mwanza MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma...

More like this

Waogeleaji wa Lake Victoria Sports Club waahidi kuing’arisha Tanzania Kimataifa

Na Mwandishi Wetu Jumla ya waogeleaji sita  chipukizi wa Lake Victoria Sports Club  ya jijini...

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...