Yanga yaingilia ugomvi wa Mangungu na mshabiki Simba

Na Mwandishi Wetu

UONGOZI wa Klabu ya Yanga umesema umesikitishwa na kitendo cha vurugu alichofanyiwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu na mashabiki wa klabu hiyo jana Februari 1, 2025 baada ya mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya ES Tunis ya Tunisia iliyochezwa kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo  ambao ilitoka sare ya mabao 2-2, licha ya kuongoza  kipindi chote cha kwanza ikienda mapumziko  ikiwa mbele kwa mabao 2-0, baadhi ya mashabiki walimvamia kiongozi huyo kwa kutaka kumpiga kutokana na kukasirishwa na matoke ohayo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Ofisa Habari wa Yanga leo, Ally Kamwe, amesema vitendo vya aina hiyo, akiviita vya kihuni, havikubaliki katika michezo na vinachafua taswira ya soka la Tanzania.

“Tulishudia moja ya tukio la ovyo kwenye mchezo wa mpira wa miguu, moja ya tukio  la kishamba zaidi kufanyika hapa kwenye ardhi yetu, moja ya tukio la kihuni. Tukio hili lilimhususisha Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, video zikisambaa zikionesha akishambuliwa na mashabiki wa klabu hiyo.

“Yanga tunakemea na kupinga vikali vitendo vya kihuni vilivyofanyika,  lakini kama klabu tunapenda kumpa pole Mwenyekiti Mangungu na viongozi wote wa Simba waliokumbana na ghasia hiyo,” amesema Kamwe.

spot_img

Latest articles

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

Vunjabei, Sara kuisaka heshima ya Tanzania One ulingoni

Na Winfrida Mtoi MABONDIA wa ngumi za kulipwa, Halima Ramadhani maarufu Vunjabei na Sara Alex...

More like this

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...