Yanga yaingilia ugomvi wa Mangungu na mshabiki Simba

Na Mwandishi Wetu

UONGOZI wa Klabu ya Yanga umesema umesikitishwa na kitendo cha vurugu alichofanyiwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu na mashabiki wa klabu hiyo jana Februari 1, 2025 baada ya mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya ES Tunis ya Tunisia iliyochezwa kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo  ambao ilitoka sare ya mabao 2-2, licha ya kuongoza  kipindi chote cha kwanza ikienda mapumziko  ikiwa mbele kwa mabao 2-0, baadhi ya mashabiki walimvamia kiongozi huyo kwa kutaka kumpiga kutokana na kukasirishwa na matoke ohayo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Ofisa Habari wa Yanga leo, Ally Kamwe, amesema vitendo vya aina hiyo, akiviita vya kihuni, havikubaliki katika michezo na vinachafua taswira ya soka la Tanzania.

“Tulishudia moja ya tukio la ovyo kwenye mchezo wa mpira wa miguu, moja ya tukio  la kishamba zaidi kufanyika hapa kwenye ardhi yetu, moja ya tukio la kihuni. Tukio hili lilimhususisha Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Murtaza Mangungu, video zikisambaa zikionesha akishambuliwa na mashabiki wa klabu hiyo.

“Yanga tunakemea na kupinga vikali vitendo vya kihuni vilivyofanyika,  lakini kama klabu tunapenda kumpa pole Mwenyekiti Mangungu na viongozi wote wa Simba waliokumbana na ghasia hiyo,” amesema Kamwe.

spot_img

Latest articles

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

More like this

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...