Kipa wa zamani Yanga afariki dunia

Na Winfrida Mtoi

KIPA wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Peter Manyika amefariki dunia leo Januari 26, 2025, wakati akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya St. Monica, jijini Dar es Salaam.

Familia kupitia mtoto wake, Manyika JR imethibitisha kuwa baba yake amefariki, mwili umehifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala, na msiba upo nyumbani kwao Mbezi.

Manyika atakumbukwa katika historia ya soka nchini kama miongoni mwa makipa bora waliojipatia heshima kubwa nchini akiwa na Yanga na timu ya Taifa kuanzia miaka ya mwishoni mwa miaka ya 1980 na 1990.

Mwaka 1999 aliiongoza Yanga kutwaa ubingwa wa Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati mwaka 1999 nchini Uganda.

Baada ya kustaafu soka la ushindani, hakuachana na mchezo huo, aliamua kujikita katika ukocha wa makipa na kuendeleza vipaji, akifanya kazi na klabu  mbalimbali zikiwamo Ihefu, Fountain Gate na timu za taifa za vijana.

Mwaka 2019 klabu yake za zamani, Yanga ilimpa jukumu la kuwanoa makipa wa timu hiyo akichukua nafasi ya Juma Pondamali, kipindi hicho alikuwa ni Metecha Mnata, Faroukh Shikalo, Klaus Kindoki na Ramadhan Kabwili.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

MD Twange aeleza kutoridhishwa na kasi ya Mkandarasi wa mradi wa Hale

📍Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme 📍Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa...

More like this

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...