Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi

WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa kikosi hicho Laurindo Aurelio maarufu Depu akitupia bao moja katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Januari 19,2025 kwenye dimba la KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Depu raia wa Angola ni usajili mpya ndani ya kikosi cha Wananchi ambapo ameonekana kuanza vizuri kwani aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Maxi Nzengeli lakini alifanyikiwa  kufunga na kutoa pasi ya  bao.

Wachezaji wengine waliofunga katika mchezo huo ni Mohammed Damaro, Duke Abuya, Pacome Zouzoua, Prince Dube na Mudathir Yahya.

Matokeo hayo yameifanya Yanga kufikisha pointi 19 na kuongoza msimamo wa Ligi Kuu, ikiwa imecheza michezo saba ikishinda sita na kutoka sare mmoja, huku Mashujaa ikibaki nafasi ya tano na pointi 13 baada ya michezo 10.

Baada mchezo huo Wanajangwani hao wanajiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi ambapo wanatarajiwa kukutana na Al Ahly  nchini Misri, Ijumaa Januari 23,2025.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

MD Twange aeleza kutoridhishwa na kasi ya Mkandarasi wa mradi wa Hale

📍Ni ule wa kuboresha kituo cha kufua umeme 📍Amuagiza kuongeza kasi ya utekelezaji wa...

More like this

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...