Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi

WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa kikosi hicho Laurindo Aurelio maarufu Depu akitupia bao moja katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Januari 19,2025 kwenye dimba la KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Depu raia wa Angola ni usajili mpya ndani ya kikosi cha Wananchi ambapo ameonekana kuanza vizuri kwani aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Maxi Nzengeli lakini alifanyikiwa  kufunga na kutoa pasi ya  bao.

Wachezaji wengine waliofunga katika mchezo huo ni Mohammed Damaro, Duke Abuya, Pacome Zouzoua, Prince Dube na Mudathir Yahya.

Matokeo hayo yameifanya Yanga kufikisha pointi 19 na kuongoza msimamo wa Ligi Kuu, ikiwa imecheza michezo saba ikishinda sita na kutoka sare mmoja, huku Mashujaa ikibaki nafasi ya tano na pointi 13 baada ya michezo 10.

Baada mchezo huo Wanajangwani hao wanajiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi ambapo wanatarajiwa kukutana na Al Ahly  nchini Misri, Ijumaa Januari 23,2025.

spot_img

Latest articles

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

More like this

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...