JBIC na JICA waahidi ushirikiano kwa ETDCO

Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya Japan Bank for International Cooperation (JBIC) pamoja na Japan International Cooperation Agency (JICA) zimeahidi kushirikiana na Kampuni ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Umeme (ETDCO) katika utekelezaji wa miradi yake ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umeme nchini Tanzania, ikiwemo uwekezaji wa kimkakati.

Wakizungumza katika vikao kazi vilivyofanyika, jijini Tokyo, Japan, viongozi kutoka JBIC na JICA wameeleza dhamira yao ya kushirikiana na ETDCO katika nyanja za uwekezaji, uhamishaji wa teknolojia na utekelezaji wa miradi ya Nishati nchini Tanzania itakayo saidia kuimarisha hali ya upatikanaji wa Nishati ya umeme.

Vikao kazi hivyo ni mwendelezo wa mafanikio ya ETDCO katika Maonesho ya Dunia (Expo 2025) yanayofanyika Osaka, Japan, ambapo Kampuni hiyo inaendelea kujitangaza kimataifa na kuimarisha mtandao wa ushirikiano kwa ajili ya kuharakisha utekelezaji wa miradi yake.

spot_img

Latest articles

NIRC kutekeleza miradi 30 ya umwagiliaji, kufungua maelfu ya ajira kwa vijana

Na Mwandishi Wetu, Dodoma SERIKALI kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imezindua mkakati wa...

TTB yampokea Mr. Alaya anayewania Guinness World Records

Na Mwandishi Wetu TANZANIA imepokea mhamasishaji amani duniani, Saddam Alaya (Mr. Alaya), ambaye anatekeleza...

VETA yaleta suluhisho la kupiga mpunga kwa wakulima

Na Mwandishi Wetu, Dodoma MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imekuja na...

TAMKU yatanua uwekezaji, kujenga kiwanda cha korosho Tunduru

Na Mwandishi Wetu CHAMA Kikuu cha Ushirika cha TAMKU kimeanza kutekeleza mkakati wa kupanua...

More like this

NIRC kutekeleza miradi 30 ya umwagiliaji, kufungua maelfu ya ajira kwa vijana

Na Mwandishi Wetu, Dodoma SERIKALI kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imezindua mkakati wa...

TTB yampokea Mr. Alaya anayewania Guinness World Records

Na Mwandishi Wetu TANZANIA imepokea mhamasishaji amani duniani, Saddam Alaya (Mr. Alaya), ambaye anatekeleza...

VETA yaleta suluhisho la kupiga mpunga kwa wakulima

Na Mwandishi Wetu, Dodoma MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imekuja na...