Kidao aondolewa  TFF

Na Mwandishi Wetu

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limemteua Oscar Mirambo kuwa Kaimu Katibu Mkuu akichukua nafasi ya Kidao Wilfred.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Septemba 24, 2025 na Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Cliford Ndimbo, mkataba wa Kidao unafikia tamati Septemba 30 mwaka.

“Uteuzi wa Mirambo ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, utaanza rasmi tarehe 1 Oktoba 2025,” imesema taarifa hiyo.

Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Oscar Mirambo

Kidao amedumu katika nafasi hiyo miaka nane, kwa mara ya kwanza  aliteuliwa mwaka 2017, hivyo kukaa  kwenye kiti hicho kwa mihula mitatu tofauti ya uongozi wa Rais wa TFF, Wallace Karia.

spot_img

Latest articles

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

Waangalizi wa Uchaguzi watakiwa kutoingilia mchakato wa Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAANGALIZI wa Uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wametakiwa kuzingatia sheria...

More like this

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...