Simbu afichua siri ya ushindi

Na Winfrida Mtoi

Bingwa wa Dunia wa mbio za Marathoni za kilomita 42, ambaye ni Askari wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ), Sajenti Alphonce Simbu, amesema si rahisi kushinda lakini ukijiandaa, kujituma na kufanya juhudi, unafanikiwa.

Simbu ambaye ameshinda medali ya dhahabu katika mashindano yaliyofanyika Tokyo, nchini Japan, amewaslli leo saa 9:13 alfajiri na kupokelewa na watu mbalimbali pamoja na familia yake.

Akizungumza baada ya kuwasili amewataka wanamichezo wa kitanzania hasa riadha, kufanya juhudi na kujiandaa na wasikate tamaa katika kufikia ndoto zao.

“Niwasihi tu wachezaji wa kitanzania kwamba wanaweza na wasikate tamaa kwa sababu ukikata tamaa unaweza usifikie ndoto zako. Niwaambie tu juhudi, kujituma na nidhamu zinasaidia,” amesema Simbu.

Simbu aliibuka mshindi akitumia muda wa 2:09:48, akiwashinda wanariadha 89 kutoka nchi mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...