Baraza ataja mbinu za kuimaliza Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa timu ya Pamba Jiji, Francis Baraza amesema hana presha yoyote kuelekea mchezo wao wa  kesho dhidi ya Yanga  kutokana na alivyojipanga, akijivunia mbinu zake.

Amesema anaamini ana wachezaji wazuri wanaoweza kutoa ushindani kwa Yanga, hivyo ataingia uwanjani kuonesha burudani ya soka  kwa kushambulia na si kwenda kuzuia ‘kupaki basi’  kama wengi wanavyotarajia.

“Mifumo yote mimi nitaipiga, mshakuwa na ile kuwa tutapoteza lakini dakika 90 zitaongea. Najua Yanga ni mabingwa, ni timu imechukua mara nne. Ila mimi sina presha, nikiweka presha nitawaumiza wachezaji wangu,” amesema Baraza.

Kocha huyo raia wa Kenya, amesema kwa kawaida anapokutana na timu kubwa huwa anatumia nafasi hiyo kuwapa fursa wachezaji wake hasa wadogo ili kuonesha uwezo wao na kuthibisha hilo kesho atamuanzisha kijana wa umri chini ya miaka 20 (U -20).

Ameeleza kuwa pamoja na kuwa nchini Kenya lakini anafuatilia Ligi ya Tanzania, msimu mzima uliopita ameifuatilia mechi za Pamba na anajua ni sehemu gani ina shida anaendelea kurekebisha.

 Yanga na Pamba zitakutana katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam, ikiwa ni  mechi ya kwanza ya msimu mpya  kwa Yanga ambayo ni bingwa mtetezi na mchezo wa pili wa Pamba.

spot_img

Latest articles

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...

Benki ya CRDB yaja na ‘Benki Kimpango Wako’ yaahidi huduma bora zaidi mwaka 2026

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake ya mwaka 2026 inayoitwa ‘Benki Kimpango...

More like this

ETDCO yaahidi kukamilisha Mradi wa Umeme katika vitongoji 372 Ruvuma kwa wakati

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji...

Wadau sekta ya Hali ya Hewa wajadili utabiri wa Masika 2026

Na Mwandishi Wetu WADAU kutoka sekta mbalimbali nchini wamekutana kujadili utabiri wa msimu wa...

WMA yafunga Mtambo wa kisasa unaohakiki Dira za Maji Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Vipimo (WMA) umesimika mtambo wa kisasa wa kidijitali wa...