Baraza ataja mbinu za kuimaliza Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa timu ya Pamba Jiji, Francis Baraza amesema hana presha yoyote kuelekea mchezo wao wa  kesho dhidi ya Yanga  kutokana na alivyojipanga, akijivunia mbinu zake.

Amesema anaamini ana wachezaji wazuri wanaoweza kutoa ushindani kwa Yanga, hivyo ataingia uwanjani kuonesha burudani ya soka  kwa kushambulia na si kwenda kuzuia ‘kupaki basi’  kama wengi wanavyotarajia.

“Mifumo yote mimi nitaipiga, mshakuwa na ile kuwa tutapoteza lakini dakika 90 zitaongea. Najua Yanga ni mabingwa, ni timu imechukua mara nne. Ila mimi sina presha, nikiweka presha nitawaumiza wachezaji wangu,” amesema Baraza.

Kocha huyo raia wa Kenya, amesema kwa kawaida anapokutana na timu kubwa huwa anatumia nafasi hiyo kuwapa fursa wachezaji wake hasa wadogo ili kuonesha uwezo wao na kuthibisha hilo kesho atamuanzisha kijana wa umri chini ya miaka 20 (U -20).

Ameeleza kuwa pamoja na kuwa nchini Kenya lakini anafuatilia Ligi ya Tanzania, msimu mzima uliopita ameifuatilia mechi za Pamba na anajua ni sehemu gani ina shida anaendelea kurekebisha.

 Yanga na Pamba zitakutana katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam, ikiwa ni  mechi ya kwanza ya msimu mpya  kwa Yanga ambayo ni bingwa mtetezi na mchezo wa pili wa Pamba.

spot_img

Latest articles

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

More like this

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...