NIDA yawasajili watu wenye mahitaji maalum Temeke

Na Tatu Mohamed

KATIKA kuadhimisha Siku ya Utambulisho Duniani, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imetoa huduma maalum ya usajili kwa watu wenye mahitaji maalum katika Halmashauri ya Temeke, jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata kitambulisho cha Taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji Vitambulisho NIDA, Edson Guyai, alisema lengo la serikali ni kuhakikisha wananchi wote, wakiwemo wenye changamoto za ulemavu na mahitaji mengine maalum, wanapata fursa ya kusajiliwa.

“Leo tumewafikia watu wenye mahitaji maalum kama sehemu ya maadhimisho haya. Ni wajibu wetu kuhakikisha kila mmoja anapata kitambulisho cha Taifa kwa kuwa shughuli zote za kijamii na kiuchumi zinahitaji utambulisho huu,” alisema Guyai.

Aidha, aliwataka wananchi kwa ujumla kuhakikisha wanajisajili mapema mara tu wanapofikisha miaka 18 ili kupunguza msongamano wa watu katika vituo vya usajili vya NIDA.

“Ukifikisha miaka 18, nenda ukajisajili mara moja. Kitambulisho hiki kinakutambulisha na kinakuwezesha kupata huduma mbalimbali muhimu za kijamii,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Afisa Ustawi wa Jamii na Mratibu wa Watu Wenye Ulemavu wa Halmashauri ya Temeke, Restuta Bujiku, aliishukuru NIDA kwa fursa hiyo na kuwataka watu wenye mahitaji maalum kuitumia ipasavyo.

“Hii ni fursa kubwa kwetu kwa kuwa mara nyingi watu wenye mahitaji maalum hawajitokezi kwa wingi kujisajili. Tunashukuru NIDA kwa kuwaleta huduma karibu na jamii yetu,” alisema Bujiku.

Mmoja wa walemavu waliosajiliwa, Mabadi Mlawa, alisema mpango huo umewasaidia kwa kuwa wengi wao walikuwa hawana vitambulisho na kulazimika kutumia vya ndugu au jamaa.

“Nawaomba walemavu wenzangu tujitoe na tujitokeze kusajiliwa. Kupata kitambulisho chetu binafsi ni hatua kubwa kwa sababu huduma nyingi sasa zinahitaji namba ya NIDA,” alisema Mlawa.

Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kauli mbiu ya ‘Kitambulisho Changu, Mwamvuli Wangu’.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...