Serikali yasitisha mchakato uchaguzi TOC

Na Mwandishi Wetu

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesitisha mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), uliopangwa kufanyika Oktoba 4, 2025 baada ya kubainika kutumia Katiba isiyo halali.

Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo leo Septemba 9,2025, imetaja sababu ya kusitishwa kwa mchakato wa uchaguzi huo ni kutokana na kukiukwa kwa taratibu, hivyo kutakiwa kuanza upya.

Taarifa hiyo imesema uamuzi huo wa kusitisha mchakato wa uchaguzi umetolewa na Waziri Pro. Palamagamba Kabudi, akiitaka TOC kuanza upya kwa kutumia Katiba inayotambulika na kisheria na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), iliyoidhinishwa Novemba 26, 2020.

“Wizara imechukua hatua hiyo kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, uwajibikaji, utawala bora na utulivu katika sekta ya michezo,” imesema.

Aidha, Wizara imesisitiza kuwa rufaa iliyowasilishwa na uongozi wa TOC kuhusu zuio la awali la Msajili wa Vyama vya Michezo, ilikataliwa, na hivyo ni lazima kufuata maelekezo ya Serikali.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...