Serikali yasitisha mchakato uchaguzi TOC

Na Mwandishi Wetu

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesitisha mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), uliopangwa kufanyika Oktoba 4, 2025 baada ya kubainika kutumia Katiba isiyo halali.

Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo leo Septemba 9,2025, imetaja sababu ya kusitishwa kwa mchakato wa uchaguzi huo ni kutokana na kukiukwa kwa taratibu, hivyo kutakiwa kuanza upya.

Taarifa hiyo imesema uamuzi huo wa kusitisha mchakato wa uchaguzi umetolewa na Waziri Pro. Palamagamba Kabudi, akiitaka TOC kuanza upya kwa kutumia Katiba inayotambulika na kisheria na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), iliyoidhinishwa Novemba 26, 2020.

“Wizara imechukua hatua hiyo kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, uwajibikaji, utawala bora na utulivu katika sekta ya michezo,” imesema.

Aidha, Wizara imesisitiza kuwa rufaa iliyowasilishwa na uongozi wa TOC kuhusu zuio la awali la Msajili wa Vyama vya Michezo, ilikataliwa, na hivyo ni lazima kufuata maelekezo ya Serikali.

spot_img

Latest articles

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri Aweso aweka kambi Dar kupambana na changamoto upungufu wa maji

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso (Mb) amefanya ziara ya kikazi katika...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

More like this

Mnyama Simba afia kwa Mkapa, Yanga, Azam kicheko

Na Winfrida Mtoi LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea leo Novemba 7, 2025 kwa michezo miwili...

Waziri Aweso aweka kambi Dar kupambana na changamoto upungufu wa maji

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso (Mb) amefanya ziara ya kikazi katika...

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...