Wauza miwani watakiwa kuzingatia sheria

Na Mwandishi Wetu

Wafanyabiashara ya miwani nchini wametakiwa kizingatia sheria na kuacha kuuza kuholela  ikiwamo kuchanganya na bidhaa nyingine kwani  miwani ni tiba, hivyo inaweza kumuathiri mtumiaji.

Hayo yamebainishwa na Msajili wa Baraza la Optometria nchini, Sebastiano Millanzi wakati wa kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya miwani, Agosti 18, 2025 katika Soko la Kabwe lililopo jijini Mbeya.

Wakati wa utoaji elimu hiyo,imebainika  kuwepo kwa baadhi ya wafanyabishara ambao hawana taaluma ya Optometria lakini wanajihusisha na uuzaji wa miwani bila kuwapima watu, huku wakiiuza pamoja na bidhaa nyingine mbalimbali za urembo kinyume na miongozo iliyopo.

Milanzi amesema ni vema anayetaka kujihusisha na biashara ya miwani azingatie sheria Optometria sura namba 23 ikiwemo kusajiliwa katika Baraza hilo.

“Kutokujua sheria sio sababu ya kuvunja sheria na ni bahati kuwa ninyi mlikuwa bado hamjapata elimu hii, hivyo kwa sasa tunawapa elimu pamoja na kuwataka kusitisha hadi pale mtakapokamilisha taratibu stahiki za usajili kuanzia ngazi ya Mganga Mkuu wa Jiji, amesisitiza  Millanzi.

Aidha ametumia wasaa huo kuziagiza mamlaka za usimamizi ngazi ya halmashauri na mkoa kuwa na muendelezo wa usimamizi shirikishi wa mara kwa mara na kutoa elimu endelevu kwa wananchi.

Kwa upande wao wafanyabiashara hao wamekiri kufanya biashara hiyo bila kujua kuwa wanakiuka taratibu, hivyo wakaahidi kuzingatia maagizo yaliyotolewa kwao ya kuanza taraibu za usajili.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...