Taifa Stars yaandika historia CHAN, yatinga robo fainali kibabe

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeandika historia kwa mara kwanza kwa kutinga robo fainali ya michuano ya CHAN ikiichapa Madagascar mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa leo Agosti 9, 2025 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Stars iliyopo kundi B imefikisha pointi tisa, huku ikiwa imebakiwa na mechi moja dhidi ya Afrika ya Kati ambayo inaburuza mkia katika kundi hilo.

Taifa Stars imekuwa timu ya kwanza kutinga robo fainali katika michuano hiyo ikiwa haijapoteza mechi hata moja katika tatu ilizocheza.

Ilianza mechi ya ufunguzi ya michuano hiyo kwa kuitandika Burkina Faso mabao 2-0, ikaichapa Mauritania bao 1-0 na leo kuikung’uta Madagascar 2-1, mechi zote zikipigwa dimba la Mkapa.

Ukiangalia msimamo ulivyo katika kundi B, Burkina Faso pekew ndiyo ina uwezo wa kufikisha kufikia alama tisa kutokana na kucheza mechi mbili na kupata pointi tatu, imebakiza michezo miwili.

Nafasi ya pili ipo Mauritania na pointi nne ikicheza mechi tatu, namba tatu ni Madagascar yenye alama moja na imecheza michezo miwili, mwisho yupo Afrika ya Kati aliyecheza mechi tatu bila kupata pointi yoyote.

spot_img

Latest articles

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

More like this

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...