Taifa Stars yaandika historia CHAN, yatinga robo fainali kibabe

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeandika historia kwa mara kwanza kwa kutinga robo fainali ya michuano ya CHAN ikiichapa Madagascar mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa leo Agosti 9, 2025 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Stars iliyopo kundi B imefikisha pointi tisa, huku ikiwa imebakiwa na mechi moja dhidi ya Afrika ya Kati ambayo inaburuza mkia katika kundi hilo.

Taifa Stars imekuwa timu ya kwanza kutinga robo fainali katika michuano hiyo ikiwa haijapoteza mechi hata moja katika tatu ilizocheza.

Ilianza mechi ya ufunguzi ya michuano hiyo kwa kuitandika Burkina Faso mabao 2-0, ikaichapa Mauritania bao 1-0 na leo kuikung’uta Madagascar 2-1, mechi zote zikipigwa dimba la Mkapa.

Ukiangalia msimamo ulivyo katika kundi B, Burkina Faso pekew ndiyo ina uwezo wa kufikisha kufikia alama tisa kutokana na kucheza mechi mbili na kupata pointi tatu, imebakiza michezo miwili.

Nafasi ya pili ipo Mauritania na pointi nne ikicheza mechi tatu, namba tatu ni Madagascar yenye alama moja na imecheza michezo miwili, mwisho yupo Afrika ya Kati aliyecheza mechi tatu bila kupata pointi yoyote.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...