Salum Mwalimu mgombea urais Chaumma, Devota Minja mgombea mwenza

Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), kimemtangaza Salum Mwalimu kuwa mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Uamuzi huo umetangazwa leo Agosti 7, 2025 na Naibu Katibu Mkuu wa Chaumma, Benson Kigaila kwenye Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Amesema jina la Mwalimu lilipendekezwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho yenye jukumu la kuleta mapendekezo ya jina la mgombea urais Tanzania na Zanzibar katika kikao kilichofanyika jana.

Baada ya kutangazwa mgombea urais chama hicho, Mwalimu amemteua Devotha Minja kuwa mgombea mwenza katika uchaguzi mkuu.

Salum Mwalimu na Devotha ni wanasiasa waliojiunga na chama hicho mwaka huu wakitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambako waliwahi kuwa katika nafasi mbalimbali za uongozi.

Katika hatua nyingine Chaumma kimeidhinisha rasmi ilani yake ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

spot_img

Latest articles

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

Senegal yavuliwa ubingwa wa AFCON 2025, wapewa Morocco

Na Mwandishi Wetu SENEGAL imevuliwa ubingwa  wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada...

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...

Vijana 3,967 waomba uwezeshaji kupitia Go Green na IMBEJU ya CRDB Bank Foundation

Na Mwandishi wetu JUMLA ya vijana 3,967 kutoka maeneo mbalimbali nchini wamewasilisha maombi ya...

More like this

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

Senegal yavuliwa ubingwa wa AFCON 2025, wapewa Morocco

Na Mwandishi Wetu SENEGAL imevuliwa ubingwa  wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada...

Yanga kuikabili TRA bila Depu, kocha aeleza ugumu ulipo

Na Mwandishi Wetu WAKATI Yanga ikitarajiwa kushuka dimbani kesho Machi 18, 2026  kuikabili TRA United katika Ligi...