Salum Mwalimu mgombea urais Chaumma, Devota Minja mgombea mwenza

Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), kimemtangaza Salum Mwalimu kuwa mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Uamuzi huo umetangazwa leo Agosti 7, 2025 na Naibu Katibu Mkuu wa Chaumma, Benson Kigaila kwenye Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Amesema jina la Mwalimu lilipendekezwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho yenye jukumu la kuleta mapendekezo ya jina la mgombea urais Tanzania na Zanzibar katika kikao kilichofanyika jana.

Baada ya kutangazwa mgombea urais chama hicho, Mwalimu amemteua Devotha Minja kuwa mgombea mwenza katika uchaguzi mkuu.

Salum Mwalimu na Devotha ni wanasiasa waliojiunga na chama hicho mwaka huu wakitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambako waliwahi kuwa katika nafasi mbalimbali za uongozi.

Katika hatua nyingine Chaumma kimeidhinisha rasmi ilani yake ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...