Mfanyabiashara ahukumiwa jela maisha kwa kumbaka mtoto wa miaka minne

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Wilaya ya Mbozi imemtia hatiani na kumhukumu kifungocha maisha gerezani, mfanyabiashara Athuman Mtibwa (35) na kulipa kiasi cha fidia milioni moja kwa mwathirika kwa kosa la kubaka mtoto wa miaka minne.

Kwa mujibu wa taarifa iliyokwa kwenye mtandao wa kijamii  @polisi.tanzania  Mtimbwa alikamatwa Oktoba 21, 2024 maeneo ya kiwandani Mlowo, Wilaya ya Mbozi, ilielezwa mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa alitekeleza tukio hilo la ubakaji kwa kumvizia mwanafunzi huyo wa darasa la awali akiwa anatoka shule na kumvuta kwa nguvu kisha kumuingiza katika kibanda chake cha biashara na kumbaka.

Akitoa hukumu hiyo Julai 29, 2025 kesi namba 32392 ya mwaka 2024, Hakimu mkazi wa Wilaya ya Mbozi,Nemes Chami alisema Mahakama imejiridhisha pasipo na shaka ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri na kumtia hatiani mtuhumiwa huyo.

“Mshtakiwa amehukumiwa kifungo pamoja na fidia hiyo ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaojihusisha na vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto,”

spot_img

Latest articles

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

More like this

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...