DED Mkalama: Wizara ya Nishati endeleeni kusimamia ufanisi wa miradi ya nishati

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida, Asia Juma Messos ametoa wito kwa Wizara ya Nishati kuendelea kusimamia vyema Taasisi zake ili ziendelee kutekeleza miradi ya Sekta ya Nishati kwa ufanisi na hivyo kuleta maendeleo kwa Wananchi.

Messos amesema hayo Agosti 6, 2025 wakati alipoitembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ( Nanenane) Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa Wananchi ikiwemo miradi ya umeme na Gesi Asilia hivyo Wizara iendelee kuzisimamia Taasisi zake, ziweze kutekeleza miradi hiyo kwa ufanisi.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Mkalama pia ametembelea Mabanda ya Taasisi za Wizara ambazo ni TANESCO, REA, EWURA, PURA, TPDC, PBPA na TGDC ili kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa katika Maonesho hayo.

Katika ziaza hiyo Messos ameambatana na Katibu Tawala Wilaya ya Mpwapwa, Michael Maganga, Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala kutoka Wizara ya Kilimo, Eliasifu Mlay.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...