DED Mkalama: Wizara ya Nishati endeleeni kusimamia ufanisi wa miradi ya nishati

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida, Asia Juma Messos ametoa wito kwa Wizara ya Nishati kuendelea kusimamia vyema Taasisi zake ili ziendelee kutekeleza miradi ya Sekta ya Nishati kwa ufanisi na hivyo kuleta maendeleo kwa Wananchi.

Messos amesema hayo Agosti 6, 2025 wakati alipoitembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ( Nanenane) Jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa Serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa Wananchi ikiwemo miradi ya umeme na Gesi Asilia hivyo Wizara iendelee kuzisimamia Taasisi zake, ziweze kutekeleza miradi hiyo kwa ufanisi.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Mkalama pia ametembelea Mabanda ya Taasisi za Wizara ambazo ni TANESCO, REA, EWURA, PURA, TPDC, PBPA na TGDC ili kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa katika Maonesho hayo.

Katika ziaza hiyo Messos ameambatana na Katibu Tawala Wilaya ya Mpwapwa, Michael Maganga, Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala kutoka Wizara ya Kilimo, Eliasifu Mlay.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...