Tamasha la Singeli Agosti 2 wasanii kutoa burudani ya Kimataifa

Na Winfrida Mtoi

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amesema wamefanya maandalizi yakutosha ya Tamasha la Muziki wa Singeli kuhakikisha wageni waliokuja nchini kwa ajili ya michuano ya CHAN wanapata burudani ya kipekee.

Akizungumza na waandishi wa leo Julai 31, 2025, jijini Dar es Salaam akielezea maandalizi ya tamasha hilo litakalofanyika kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Msingwa amesema wageni wakitoka kuangalia soka wanahamia kucheza singeli upande wa pili.

” Hii ni moja ya shughuli ambayo inafanywa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika kipindi hiki cha CHAN. Tumeona tusinde kinyonge baada ya mechi ya Taifa Stars na Burkina Faso, tutashusha bonge la tamasha la singeli ili wageni waliotoka nchi mbalimbali waje waone muziki wenye asili ya Kitanzania,” amesema Msingwa.

Aidhs ameeleza kuwa katika kuendelea kuupaisha muziki huo kimataifa, Serikali imeanza kutuma maandiko kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni(UNESCO) ili kuutambua kama urithi wa Taifa.

Msingwa amesema kwa sasa Tanzania hakuna muziki unaopendwa watu wengi, wenyeji na wagenj kama ilivyo Singeli.

“Tumegundua hakuna ‘vibes’, linalofikia muziki wa singeli katika muziki wote Tanzania. Wazungu wanachanganyikiwa ukipigwa, wanacheza na kuimba huku hawajui wanaimba nini.

” Ni muziki unaozalisha ajira kwa vijana, lazima tuupromote, tuulinde na maeneo wanayofanya vibaya tutawarekebisha ili dunia ijue kuwa asili ya singeli ni Tanzania,” amesema Msingwa.

Kwa upande wake msanii wa Singeli, Manfongo, ameeleza walivyofurahishwa na fursa hiyo na kuahidi kutoa burudani kabambe kwa wageni na watanzania watakaofika siku hiyo.

“Niwaambie tu watanzania wenzangu wajitokeze kwa wingi siku ya ufunguzi wa CHAN na sisi tumejipanga vizuri kuwapa burudani ya kutosha kwenye tamasha la Singeli,”

Wasanii zaidi ya 15, wajarajiwa kutoa burudani siku hiyo, wakiwamo Dogo Paten, Miso Misondo, Wamoto Musik, Mbosso, Shoro Mwamba na Meja Kunta.

spot_img

Latest articles

IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja...

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...

Wanahabari watakiwa kuweka usawa katika uandishi wa mabadiliko ya tabianchi

Na Tatu Mohamed MWAKILISHI wa kimataifa kutoka ActionAid International, Teresa Anderson, amesema ipo haja...

More like this

IST Festival yatumika kunadi mitaji nafuu kwa vijana

Na Mwandishi Wetu TAMASHA la IST Festival lililofanyika jana Februari 14, 2026 kwenye viwanja...

Taliss – IST Swimming Championships yawavuta wenye mahitaji maalumu

Na Winfrida Mtoi MASHINDANO ya mchezo wa kuogelea 'Taliss -IST Championship' yameanza leo Februari 14,...

CRDB na Costech watenga Sh. Bilioni 4.6 kuwezesha mitaji kwa vijana wabunifu

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia TUME ya Sayansi na...