Tyson wa Bongo afunga mtaa 

Na  Winfrida  Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa Hassan Ndonga maarufu Tyson wa Bongo amefunga  Mtaa wa Banda Mabibo, Dar es Salaam kutokana na wingi wa mashabiki waliojitokeza kumsapoti katika maandalizi ya pambano lake la  Dar Boxing Derby  dhidi ya Mohammed Mpombo  litakalofanyika Julai 26,2025, Viwanja Vya Leaders Club. 

Tyson ambaye anatokea kambi ya Makatuni Pesa, ameweka wazi kuwa hajawahi kufeli katika mapambano yake mengi aliyocheza na kuwahakikishia ushindi mashabiki zake.

“Ukizungumzia K.O huwa inakuja yenyewe ‘automatic, sababu hata ukiangalia mapambano yangu mawili ya mwisho,  la kwanza nilikuwa nacheza raundi nane lakini nikampiga mtu  raundi ya pili, jingine nilicheza Morogoro katika raundi nane nikampiga mpinzani wangu katika raundi ya sita,” ametamba.

Amewaambia mashabiki zake wasisite kujitokeza siku hiyo kwa kuhofia kwani yeye amejipanga  kushinda kutokana na maandalizi anayofanya.

Mmoja wa mashabiki wa bondia huyo,  Hamza. Mohammed, amesema anamkubali bondia wao kwa sababu siku zote hawana kazi mbovu na ameshuhudia hilo mazoezini  na ulingo utasema siku hiyo.

spot_img

Latest articles

Azam yamrejesha Manula

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Azam imemrejesha golikipa wao wa zamani, Aishi Manula akitokea Simba...

Fountain Gate FC yakwepa kushuka daraja

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Fountain Gate  imefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu  Tanzania Bara kwa msimu ujao...

Rais Samia kuzindua Dira ya Taifa ya 2050

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Dira ya Maendeleo ya Taifa...

NIT yaendelea na mafunzo ya Urubani, yawataka vijana kuchangamkia fursa

Na Tatu Mohamed CHUO cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimeanza rasmi kutoa mafunzo ya...

More like this

Azam yamrejesha Manula

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Azam imemrejesha golikipa wao wa zamani, Aishi Manula akitokea Simba...

Fountain Gate FC yakwepa kushuka daraja

Na Mwandishi Wetu Klabu ya Fountain Gate  imefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu  Tanzania Bara kwa msimu ujao...

Rais Samia kuzindua Dira ya Taifa ya 2050

Na Mwandishi Wetu Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Dira ya Maendeleo ya Taifa...