Ofisi ya Mwanasheria Mkuu Kusimamia Ubora wa Mikataba ya Umma kwa Maslahi ya Taifa

Na Tatu Mohamed

OFISI ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kutoa ushauri wa kisheria kwa taasisi za umma ili kuhakikisha mikataba inayosainiwa na serikali inakuwa na ubora, inatekelezwa ipasavyo na inazinufaisha jamii.

Kauli hiyo imetolewa Julai 07, 2025 na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Samwel Maneno alipokuwa akizungumza katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere.

“Tunaendelea kuzipa ushauri taasisi za umma ili kuwa na mikataba yenye ubora na kuhakikisha utekelezaji wake unafanyika kwa mujibu wa makubaliano,” alisema Maneno.

Ameongeza kuwa maonesho ya Sabasaba ni jukwaa muhimu kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutoa huduma kama ushauri wa kisheria, kushughulikia malalamiko ya wananchi, pamoja na elimu kuhusu sheria zilizofanyiwa marekebisho, toleo la mwaka 2023, ambazo zimeanza kutumika rasmi kuanzia Julai 1, 2025.

“Katika sheria 446 zilizofanyiwa urekebishaji, zaidi ya sheria 300 tayari zinapatikana kwa lugha ya Kiswahili, jambo ambalo linaongeza uelewa wa wananchi kuhusu sheria,” alifafanua.

Katika ziara yake, Naibu Mwanasheria Mkuu pia alitembelea mabanda ya Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria na Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo, kujionea namna taasisi hizo zinavyoshiriki katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Maonesho ya Sabasaba 2025 yamezinduliwa rasmi na Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, na yanatarajiwa kumalizika Julai 13, 2025.

spot_img

Latest articles

Makamu wa Rais atangaza kujiuzulu

Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kuanzia...

RAIS SAMIA AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUJIANDAA NA UDHIBITI WA ATHARI ZA ELNINO

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

JNHPP kuongeza Umeme wa Gridi ya Taifa kwa asilimia 45

Na Tatu Mohamed BWAWA la Julius Nyerere (JNHPP) linatarajiwa kuongeza kwa kiasi kikubwa uwezo...

More like this

Makamu wa Rais atangaza kujiuzulu

Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kuanzia...

RAIS SAMIA AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUJIANDAA NA UDHIBITI WA ATHARI ZA ELNINO

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...