Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kuanzia Septemba 4, 2026.
Katika ukurasa wake wa Instagram, Dk. Nchimbi ameandika kuwa: “Leo tarehe 25 Agosti 2026, nimemwandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kumjulisha kuwa nimeamua kustaafu siasa na utumishi wa umma. Hivyo, nitajiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuzingatia Ibara ya 50(2)(c) ikisomwa kwa pamoja na Ibara ya 149(2) ya Katiba, kuanzia tarehe 04 Septemba 2026.



