FCC yawahamasisha wananchi kulinda Afya na Haki zao dhidi ya Bidhaa Bandia

Na Tatu Mohamed

TUME ya Ushindani (FCC) imewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kulinda afya na usalama wao kwa kujiepusha na bidhaa bandia, huku ikisisitiza umuhimu wa elimu kwa jamii kuhusu haki za walaji na mazingira salama ya biashara.

Kauli hiyo ilitolewa Julai 4, 2025 na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Hadija Ngasongwa, alipotembelea Banda la Viwanda na Biashara katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

“FCC haishughulikii tu makampuni au wawekezaji, bali inalinda afya ya jamii nzima. Tuna jukumu la kuhakikisha wananchi wanapata bidhaa salama, bora na zinazokidhi viwango vya kisheria,” alisema Hadija.

Alibainisha kuwa moja ya changamoto kubwa kwa jamii ni upatikanaji wa bidhaa bandia, ambazo zinaweza kuleta madhara ya kiafya, kiuchumi na kijamii.

“Elimu ni silaha kuu. Tunawahimiza wananchi kufika kwenye banda letu kujifunza namna ya kuzitambua bidhaa bandia,” aliongeza.

Hadija alisema FCC imekuwa ikitoa elimu kwa walaji kuhusu haki zao, ikiwa ni pamoja na kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi sahihi ya manunuzi, kudai stakabadhi, na kuripoti bidhaa zisizo salama.

Pia aliwahamasisha wananchi wa kipato cha chini kuchangamkia fursa zinazopatikana kupitia maonyesho ya Sabasaba kwa kushirikiana na kampuni mbalimbali ili kukuza biashara zao kwa njia halali.

“Tunataka jamii ielewe kuwa kulinda haki ya mteja ni kulinda jamii nzima. Ndiyo maana tumeleta wataalamu wetu kutoa elimu moja kwa moja hapa Sabasaba,” alisema.

Kwa ujumla, FCC inatumia jukwaa la Sabasaba sio tu kusimamia ushindani wa haki, bali kama daraja la kuunganisha elimu, usalama wa jamii na kukuza mazingira bora ya biashara kwa Watanzania wote.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...