Rais Samia alitaka Jeshi la Polisi  kukomesha matukio ya watu kupotea, ataja sababu  ongezeko la deni la Taifa

Na Mwandishi Wetu

Rais  Samia Suluhu Hassan, ameliagiza  Jeshi la Polisi nchini kuongeza  jitihada katika  kupambana na matukio ya uhalifu, hususan vitendo vya kupotea kwa watu, pamoja na kutafuta mwarobaini wa ajali za barabarani.

 “Pongezi nyingi kwa Jeshi la Polisi kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya, hatuna budi kutambua kwamba uhalifu unaozuiliwa  kwa jitihada za  Jeshi la polisi ni mkubwa kuliko  unaofanyika. Kasi ya  kuwabaini na kuwakamata wahalifu na kuwafikisha mahakamani imeongezeka. Jambo ambalo bado hatujafanikiwa vyakutosha ni ajali za barabarani lazima nazo tuendelee kuzitafutia mwarobaini wake. Aidha naliekeza jeshi la Polisi kuongeza jitihada katika kumesha matukio ya watu kupotea,”

Rais Samia ametoa maagizo hayo   leo  Juni 27, 2025 wakati akilihutubia  katika kuhitimisha  shughuli za la 12,  jijini Dodoma.

Katika hatua nyingine amebainisha kuwa mchakato wa Katiba mpya  unatarajia kuanza  kipindi kijacho cha miaka mitano kwa sababu ni miongoni mwa ahadi zinazoonekana katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2025/2030.

Ameeleza kuwa asasi za kiraia  zimekuwa huru kufanya shughuli zao  ikiwemo kukutana na kushauri Serikali na mapendekezo yao mengi yamepokelewa na kufanyiwa kazi.

Kuhusu kuongezeka kwa deni la Taifa, Rais Samia ameeleza kuwa  miongoni mwa sababu za kuongezeka  ni kutokana na fedha ambazo zilikopwa na awamu zilizopita kupokelewa na awamu hii ya sita, pamoja na kuimarika kwa dola ya Marekani jambo linalochangia kukua kwa deni la nje.

“Hadi kufikia Mei 2025 deni la Serikali lilifikia trilioni 107.7, kati ya deni  hilo deni la nje ni shilingi trilioni 72.94 na deni la ndani ni 34.76. Kuongezeka kwa deni la Serikali  kumetokana na sababu  mbalimbali, mojawapo ni kupokelewa kwa fedha za mikopo mipya na ya zamani ambayo mikataba yake iliingiwa tangu Serikali za awamu za nyuma.

“Ni vyema tukafahamu kuwa mkopo unaweza kusainiwa leo lakini fedha husika zikaanza kupokelewa baada ya maandalizi ya mradi kukamilika na mradi kuanza ili lile deni au mkopo huo uingie kwenye deni la serikali lazima serikali iwe imepokea fedha hizo huduma au vifaa tulivyokubaliana,”

“Katika awamu ya sita pamoja na kusaini mikopo mipya lakini pia tumeendelea kupokea fedha za mikopo ambayo ilisainiwa katika vipindi tofauti na kuongeza kiwango cha deni la Serikali  kwa mfano  awamu ya sita imepokea  kiasi cha shiilingi trilioni 11.3 ikiwa ni mikopo iliyosainiwa na awamu zilizopita.

Rais Samia ameeleza  kuwa  mwaka huu deni limeongezeka kwa zaidi sh 3.9 trilioni kutokana na ‘exchange rate’.

“Mfano mwezi Machi 2021 kiwango cha kubadilisha shilingi ya kitanzania dhidi ya dola za marekani ilikuwa shilingi 2,298.5 wakati mwezi Machi mwaka huu kiwango hicho kulikuwa 2,650 hivyo endapo deni la Serikali litatajwa kwa shilingi za kitanzania lazima lionekane limeongezeka,”

Akielezea mafanikio katika kipindi cha Serikali ya awamu ya sita,  amesema  uhuru wa vyombo vya habari na kutoa maoni umeongezeka kutokana na kukua kwa matumizi ya mtandao.


spot_img

Latest articles

Rais Samia ataja mafanikio Sekta ya Nishati 2020-2025

📌Ni wakati akihitimisha shughuli za Bunge jijini Dodoma 📌JNHPP, Umeme Vijijini, Umeme wa Gridi Kigoma...

Bondia Debora amtangazia vita Asia, apania kulipa kisasi

Na Winfrida Mtoi Bondia  wa ngumi za kulipwa nchini, Debora Mwenda, ametangaza vita dhidi ya...

Balozi Nchimbi ateta jambo na Mwanahabari Mkongwe, Mkurugenzi Mwenza wa Media Brains

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt John Emmanuel Nchimbi akizungumza jambo...

Dkt. Kimambo: Maafisa Ustawi wa Jamii Muhimbili zingatieni weledi, upendo na moyo wa huruma kwa wagonjwa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,(MNH) Dkt. Delilah Kimambo, amewataka...

More like this

Rais Samia ataja mafanikio Sekta ya Nishati 2020-2025

📌Ni wakati akihitimisha shughuli za Bunge jijini Dodoma 📌JNHPP, Umeme Vijijini, Umeme wa Gridi Kigoma...

Bondia Debora amtangazia vita Asia, apania kulipa kisasi

Na Winfrida Mtoi Bondia  wa ngumi za kulipwa nchini, Debora Mwenda, ametangaza vita dhidi ya...

Balozi Nchimbi ateta jambo na Mwanahabari Mkongwe, Mkurugenzi Mwenza wa Media Brains

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt John Emmanuel Nchimbi akizungumza jambo...