Bunge  laridhia marekebisho mpaka wa  Hifadhi ya Nyerere

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Bunge limeridhia ombi la Serikali la kumega sehemu ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere kwa lengo la kutatua migogoro ya mipaka na kuwezesha shughuli za maendeleo kuendelea katika mazingira rafiki kwa jamii na uhifadhi.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dk. Pindi Hazara Chana, akiwasilisha azimio hilo bungeni, amesema kuwa Serikali imeamua kumega eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 1,617 kutoka Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na kulirejesha katika Pori la Akiba Selous.

Amesema hatua hiyo imepunguza ukubwa wa hifadhi hiyo kutoka kilomita za mraba 30,893 hadi kufikia kilomita za mraba 29,276.

Akifafanua zaidi,  Chana amesema hatua hiyo inalenga kuondoa migogoro ya muda mrefu ya mipaka baina ya hifadhi hiyo, vijiji vinavyoizunguka, Pori la Akiba Selous na Jumuiya za Hifadhi za Wanyamapori za Mbarang’andu, Juhiwangumwa, Iluma, Jukumu, Magingo na Nalika.

“Kwa kufanya hivyo, tunaimarisha usalama wa maeneo yaliyohifadhiwa, tunajenga mahusiano bora kati ya wananchi na hifadhi, na kuondoa migogoro iliyodumu kwa muda mrefu,” amesema.

Aidha, Waziri huyo ameeleza kuwa marekebisho hayo ya mpaka yanalenga kulinda mfumo ikolojia muhimu unaounganisha Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na Pori la Akiba Selous, sambamba na kuhakikisha mtiririko endelevu wa maji katika Mto Rufiji, ambao ni chanzo kikuu cha uzalishaji umeme kupitia Mradi wa Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere (JNHPP).

Chana amebainisha kuwa hatua hiyo itaongeza tija kwa Taifa kwa kuimarisha shughuli za utalii, uwindaji wa kitalii katika Pori la Akiba Selous na maeneo yanayozunguka, na hivyo kuchangia mapato ya ndani kupitia sekta ya utalii.

“Kwa sasa, tunaelekea katika uboreshaji wa uhifadhi wa maliasili kwa ujumla wake – wanyamapori, mimea, mazalia ya viumbe wa majini na pia kuongeza upatikanaji wa maji kwa matumizi ya wakulima, wafugaji na wavuvi,” ameongeza.

spot_img

Latest articles

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

More like this

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...