Watumishi waaswa kuzingatia miiko, maadili ya utumishi wa Umma

Na Mwandishi Wetu

Watumishi wa Umma wameaswa kuendelea kuzingatia miiko na maadili ya utumishi wa umma, sera za nchi, sheria, kanuni na miongozo iliyopo ambayo inahitaji ukarimu, kuwapokea, kuwasikiliza na kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Maelekezo hayo yametolewa leo Juni 23,2025  na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa akihitimisha kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na Uzinduzi wa Mifumo ya Kidijiti kwa niaba ya Rais Samia Suluhu Hassan, yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.

 Majaliwa amesema ni vyema kuimarisha mikakati ya kuhamasisha wananchi kujenga utamaduni wa kutumia fursa za uwepo wa maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma ili wajitokeze kwa wingi ili waweze kupata huduma zinazotolewa na Serikali kwa haraka zaidi.

Wakati akizindua mfumo  huo amezitaka  Taasisi zote za umma kutekeleza agizo la  Rais Samia la kuhakikisha kuwa taasisi zenye mifumo na zinazoendelea kubuni mifumo inayosomana na zinaweza kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo ili kuboresha huduma ndani ya Serikali.

“Mamlaka ya Serikali Mtandao eGA hakikisheni kwamba mifumo iliyounganishwa inendelea na majukumu yake ya kubadilishana taarifa lakini pia kila anaeingia mjiridhishe kuwa ana uwezo wa kuwasiliana na yeyote alioko kwenye mfumo, amesema Majaliwa.

Vile vile Mhe. Majaliwa aliwaasa watumishi wa umma kote nchini kujisajili katika mfumo wa kidijitali wa e – wezesha, ambao unawezesha watumishi wa umma kuwekeza moja kwa moja kupitia makato ya mshahara au mapato mbalimbali ya biashara.

Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, ambayo yalianza tarehe 16 Juni, 2025 na kuhitimishwa leo tarehe 23 Juni, 2025  yameshirikisha Taasisi za Serikali 146, ikiwemo Wizara ya Fedha, pamoja na wafanyabiashara wa makundi mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...