GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu

Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers (GFA), kilichopo Kibaha mkoani Pwani, kimeweka rekodi ya uundaji magari baada ya kusheherekea kufikia utengenezaji wa idadi ya magari 4000 tangu kilipoanza uzalishaji rasmi wa magari mwaka 2020.

Akizungumza wakati wa sherehe za kuruhusu gari ya 4000 kukanyaga aridhini baada ya kuunganishwa tayari kwa kutembea ,Meneja mkuu wa kiwanda hicho ,Ezra Mereng amesema wanaishukuru Serikali kupendekeza tozo ya maendeleo ya viwanda kwenye vichwa vya Terla za magari makubwa vinavyoagizwa nchini kwa asilimia 10 ili kuvilinda viwanda vya ndani na kuchochea ununuzi wa magari yalionunganishwa nchini.

Mkurugenzi wa GF Vehicles Assemblers (GFA), Ally Karmali akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa sherehe za uundwaji wa gari ya 4000 iliyotengenezwa katika kiwanda hicho na mafundi wa ndani kutoka vyuo mbalimbali nchini kwa kushirikiana na wataalamu wa kigeni iliyofanyika Kibaha mkoani Pwani.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa GFA, All Jawad Karmali amesema wamejipanga kuhakikisha wanaongeza mtaji katika uwekezaji ili kukabiliana na soko la Afrika mashariki na kati kwa upande wa magari.

Ameeleza kuwa wanataka kuifanya Tanzania kuwa nchi moja wapo inayounganisha magari na kulisha ukanda wote wa Afrika Mashariki kutokana na mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyotengenezwa na Serikali.

Pia alizitaka tasisisi za serikali na kuagiza magari ambayo hayajaunganishwa ili kazi ya kuunganisha ifanyike na viwanda vya ndani kwa lengo la kukuza pato la Taifa na kuongeza ajira kwa watanzania, pia nchi kujipatia fedha za kigeni kwa kuuza magari yanayotoka Tanzania kwa nchi jirani.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: Mwelekeo ni elimu ya ujuzi kwa vijana kumudu soko la ajira

Na Mwandishi Wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amesema...

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...

Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja...

More like this

Rais Samia: Mwelekeo ni elimu ya ujuzi kwa vijana kumudu soko la ajira

Na Mwandishi Wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amesema...

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...