Waziri Mkuu aagiza  kukamilishwa ukarabati viwanja vya mazoezi ya CHAN  2025

Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa viwanja vitakavyotumika kufanyia mazoezi kwa timu zitakazo shiriki michuano ya CHAN Agosti 2025 na AFCON 2027 kwa ushirikiano na nchi za Kenya na Uganda na kuagiza ukamilishwaji wa ukarabati haraka.

Akizungumza  jana Juni 16, 2025 baada ya ukaguzi wa viwanja vya Gymkhana, Meja Generali Isamuhyo na kiwanja cha Chuo cha Sheria (Law School ), Majaliwa ameitaka kamati inayosimamia ujenzi huo kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa.

“Ni lazima tuwajibike kila mmoja na hasa wale ambao tumepewa majukumu, suala la AFCON na CHAN halina mjadala, tunataka michezo hii ichezwe hapa, tukishindwa watanzania hasa wapenda michezo hawatatuelewa, kila mmoja aone ana nafasi muhimu kufanya kazi hii,” amesema.

Pia  Majaliwa ameiagiza kamati hiyo kuhakikisha inasimamia ubora wa ujenzi wa kila eneo kwani hata baada ya michezo hiyo nchi itabaki na miundombinu ya viwanja ambavyo vipo kwenye ubora mkubwa.

Aidha, Waziri Mkuu ameipongeza kampuni ya ReformSports inayotekeleza ukarabati wa eneo la kuchezea la viwanja hivyo kwa kuendelea kusimamia ubora “Mnafanya kazi nzuri sana, tunawashukuru sana”

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...