Rais Mwinyi: SMZ imeweka mkazo kuifungua Pemba kiuchumi

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa Serikali imeweka mkazo maalum wa kuifungua Pemba kiuchumi kupitia ujenzi wa uwanja wa ndege, bandari na miundombinu ya barabara.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na Ujumbe Maalum wa Serikali ya Uingereza, ukiongozwa na Kate Osamor (MB), Mjumbe Maalum wa Biashara wa Serikali ya Uingereza kwa Afrika Mashariki.

Katika mazungumzo hayo Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa ujenzi wa miundombinu ya barabara umefikia asilimia 70, sambamba na maendeleo ya ujenzi wa uwanja mpya wa ndege wa Pemba pamoja na bandari.

Akizungumzia kilimo cha mwani ambacho kina mwamko mkubwa kwa wanawake wa Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa licha ya ongezeko la uzalishaji wa zao hilo, bado bei ya mwani hairidhishi kulingana na juhudi zinazowekwa na wazalishaji.

Ameutaka ujumbe huo kuangalia njia bora ya kuwawezesha wazalishaji kwa kuongeza thamani ya zao hilo.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa rai kwa ujumbe huo kwamba Zanzibar bado inahitaji wawekezaji zaidi kutoka sekta binafsi ili kufikia Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050.

Naye Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Balozi Marianne Young, amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa kasi ya maendeleo yanayofikiwa Zanzibar katika sekta mbalimbali za uchumi, na kuahidi kuendeleza ushirikiano kati ya pande hizo mbili.

spot_img

Latest articles

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...

Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini...

More like this

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...