Na Mwandishi Wetu
Licha ya kufanya kikao na uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), leo Juni 9, 2025, Klabu ya Yanga imeendelea kushikilia msimamo wake kuwa haitacheza mechi ya Juni 15,2025 dhidi ya Simba endapo hawatakapotimiziwa matakwa yao.
Kikao hicho kimefanyika ikiwa zimebaki siku sita pekee kufikia tarehe ya mchezo huo ambao awali ulitakiwa kuchezwa Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamati ya Utendaji ya Yanga leo, imesema kuwa msimamo wao hautobadilika hadi pale mahitaji yao yatakapotimizwa.

Akizungumzia yaliyojili katika kikao hicho, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almas Kasongo, amesema kuwa kikao cha leo kilikuwa kwa ajili ya kupokea matakwa ya Yanga ambayo ni manne, kujiuzulu kwa Mwenyeketi wa bodi ya ligi, kujiuzulu kwa Ofisa mtendaji mkuu wa, Katibu mkuu wa Tff na kuona bodi ya ligi kuu inakuwa chombo huru.
“Hivyo basi matakwa hayo yamepokewa na yatawasilishwa kwa shirikisho la soka nchini TFF, ila kwa mamlaka ya bodi ya ligi mpaka sasa ni mchezo upo pale pale juni 15,” amesema.