Mambo bado magumu dabi ya Kariakoo, Yanga yaikomalia Bodi ya Ligi

Na Mwandishi Wetu

Licha ya kufanya kikao na uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), leo Juni 9, 2025, Klabu ya Yanga imeendelea  kushikilia msimamo wake kuwa haitacheza  mechi  ya Juni 15,2025 dhidi ya Simba endapo  hawatakapotimiziwa matakwa yao.

Kikao hicho kimefanyika ikiwa zimebaki  siku sita pekee kufikia tarehe ya mchezo huo ambao awali ulitakiwa kuchezwa Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Kwa mujibu wa taarifa  iliyotolewa na Kamati ya Utendaji ya Yanga leo, imesema kuwa msimamo wao hautobadilika hadi pale mahitaji yao yatakapotimizwa.

Akizungumzia yaliyojili katika kikao hicho, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi,  Almas Kasongo, amesema kuwa kikao cha leo kilikuwa  kwa ajili ya   kupokea matakwa ya Yanga ambayo ni  manne,  kujiuzulu kwa Mwenyeketi wa bodi ya ligi, kujiuzulu kwa Ofisa mtendaji mkuu wa, Katibu mkuu wa Tff na kuona bodi ya ligi kuu inakuwa chombo huru.

“Hivyo basi matakwa hayo yamepokewa na yatawasilishwa kwa shirikisho la soka nchini  TFF, ila kwa mamlaka ya bodi ya ligi mpaka sasa ni mchezo upo pale pale juni 15,” amesema.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...