Prof. Ndalichako: Mazingira mazuri ya uwekezaji yamechangia ukuaji wa muko wa NSSF

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Joyce Ndalichako amesema mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyowekwa na Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa sekta binafsi yamechochea ukuaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Aidha, Prof. Ndalichako amesema ukuaji huo umepelekea thamani ya mfuko kuongezeka pamoja na michango ya wanachama.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo Agosti 17, 2023 alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya NSSF kwa mwaka 2022/23 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi wa Maendeleo ya Jamii.

Amesema kwa mwaka 2022 mfuko huo uliandikisha wanachama 233,644 hadi kufikia Juni  mwaka 2023 kulikuwa na wanachama 243,895 na matarajio ifikapo Juni 2024 ni kuwa na wanachama 277,279.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Fatuma Toufiq, ameutaka mfuko wa NSSF kuhakikisha unaongeza wanachama zaidi hasa waliopo kwenye sekta isiyo rasmi.

Akijibu hoja za wabunge, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, amewahakikishia wabunge kuzingatia maoni yao ili kuendelea kuboresha huduma kwa wanachama wake.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...