Prof. Ndalichako: Mazingira mazuri ya uwekezaji yamechangia ukuaji wa muko wa NSSF

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Prof. Joyce Ndalichako amesema mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyowekwa na Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa sekta binafsi yamechochea ukuaji wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Aidha, Prof. Ndalichako amesema ukuaji huo umepelekea thamani ya mfuko kuongezeka pamoja na michango ya wanachama.

Waziri Ndalichako ameyasema hayo Agosti 17, 2023 alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya NSSF kwa mwaka 2022/23 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi wa Maendeleo ya Jamii.

Amesema kwa mwaka 2022 mfuko huo uliandikisha wanachama 233,644 hadi kufikia Juni  mwaka 2023 kulikuwa na wanachama 243,895 na matarajio ifikapo Juni 2024 ni kuwa na wanachama 277,279.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Fatuma Toufiq, ameutaka mfuko wa NSSF kuhakikisha unaongeza wanachama zaidi hasa waliopo kwenye sekta isiyo rasmi.

Akijibu hoja za wabunge, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba, amewahakikishia wabunge kuzingatia maoni yao ili kuendelea kuboresha huduma kwa wanachama wake.

spot_img

Latest articles

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

TMA yatangaza msimu wa Kipupwe Juni hadi Agosti

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa na msimu...

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...

Wachina wanne wakamatwa kwa utekaji

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia raia wanne...

More like this

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

TMA yatangaza msimu wa Kipupwe Juni hadi Agosti

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa na msimu...

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...