Wachina wanne wakamatwa kwa utekaji

Na Mwandishi Wetu

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia raia wanne wa China kwa tuhuma za kuhusika na tukio la utekaji wa wafanyabiashara wenzao wawili, Weiyi Chen (64) na Liang Xiolo (44).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro tukio hilo lilitokea Mei 14, 2026 saa 4:30 usiku katika majengo ya PSSSF, Mtaa wa Mission, Ilala.

Watuhumiwa waliokamatwa ni Deng Anqing (49), Fan Zhong (49), Zhang Jianjun (52) na Deng Qiang (40), ambapo walikutwa na simu za wahanga pamoja na vielelezo vingine vinavyohusishwa na tukio hilo.

Inadaiwa kuwa wafanyabiashara hao  walivamiwa na kundi la watu saba na kutekwa kwa nguvu kisha kupelekwa kusikojulikana huku watuhumiwa wakidaiwa kutaka fidia ya dola za Marekani milioni 20 kutoka kwa ndugu ili kuwaachia huru.

Taarifa hiyo imesema Polisi waliweza kufuatilia magari yaliyotumika katika tukio hilo ikiwemo Toyota Alphard yenye namba bandia T.305 DRP pamoja na Toyota Harrier yenye namba T.188 DHT.

“Baada ya msako mkali uliofanyika Mei 16, 2026 Jeshi la Polisi liliwafuatilia na kuwabaini wahanga hao katika eneo la Mbezi, Kinondoni wakiwa wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao ambapo walikimbizwa hospitalini kwa matibabu huku Weiyi Chen akiendelea kupatiwa huduma kutokana na hali yake kutokuwa nzuri,”


spot_img

Latest articles

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

COASCO: Ukaguzi wa vyama vya ushirika waongeza uwazi na kuimarisha imani ya wanachama

Na Tatu Mohamed Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) limesema ukaguzi...

More like this

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...