Serikali yaja na mkakati kukabiliana na migogoro ya ardhi Morogoro

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Geophrey  Pinda amesema Serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na migogoro ya ardhi kati  ya wakulima na wafugaji katika maeneo mbalimbali hapa ikiwemo Mkoa wa Morogoro.


Ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma leo  Juni 6,  2025 wakati akijibu swali la Dk. Christine  Ishengoma Mbunge wa Vitu Maalum, aliyeuliuza ni upi mkakati wa Serikali wa kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji mkoani Morogoro?

Amesema hatua nyingine walizozichukua ni kupitia mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi (KKK) ambapo miji chipukizi kama ilivyo kwa miji ya halmashauri hupangwa, hupimwa na humilikishwa sambamba na kuweka mipango ya matumizi bora ya ardhi.

“Serikali inatambua kuwepo kwa migogoro ya wafugaji mkoani Morogoro, hata hivyo serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kukabiliana na migogoro hiyo ambapo baadhi ya hatua hizo ni  mipango ya matumizi bora za vijiji ili kubainisha maeneo ya kilimo sambamba na maeneo ya wafugaji kupitia Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi,” amesema Pinda.

Aidha, Naibu Waziri Pinda ametoa rai kwa wananchi kuhakikisha wanatumia ardhi kuendana na mipango ya matumizi iliyopangwa ili kuondoa muingiliano wa matumizi ya ardhi ambayo imekuwa chanzo cha migogoro ya wakulima na wafugaji.

spot_img

Latest articles

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

More like this

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...