Kongamano kuwafunda vijana kiuchumi laja

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Wanafunzi wa vyuo, waendesha bodaboda na makundi mengine ya vijana wanatarajia kupatiwa mafunzo yanayolenga kutambua mchango wao katika kujenga uchumi wa taifa.

Kongamano hilo litakalofanyika Dar es Salaam wakati wa Siku ya Vijana Duniani inayoadhimishwa Agosti 12 kila mwaka limeandaliwa na Shirika lisilokuwa la kiserikali linalojihusisha na uwezeshaji vijana, wanawake, watoto na watu wenye uhitaji maalumu.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 19,2023 Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Amina Said, amesema wanatambua jitihada zinazofanywa na Serikali ndiyo maana wameweka mikakati ya kuwezesha kundi hilo kwa lengo la kutatua changamoto za ajira zinazolikabili.

“Amo inalenga kumuamsha kijana kujitambua na kujua thamani yake, kijana asipojielewa na kujithamini hata ufanye vipi ni kazi bure.

“Amo inamuamsha kijana aweze kujiongoza mwenyewe na kutimiza malengo yake binafsi,” amesema Amina.

Amesema pia katika kongamano hilo vijana watapata nafasi ya kujifunza mambo mbalimbali kama kujitambua, biashara na uwekezaji, masoko, umuhimu wa kutii sheria na fursa zinazopatikana nchini na kuwataka kuchangamkia fursa hiyo kwa kujisajili.

Mkurugenzi huyo amesema watawawezesha vijana kwa kuwapatia vitendea kazi kama vile bodaboda, vyerehani, mitungi ya gesi na majiko yake.

Naye Mwalimu wa Saikolojia katika shirika hilo, Neema Bachu, amesema wataanza Dar es Salaam kisha kwenda katika mikoa mbalimbali kwa sababu tayari wamepokea maombi ya kuwafikia vijana.

Mgeni rasmi katika kongamano hilo lenye kaulimbiu isemayo ‘Uwajibikaji wetu ndio uhai wa uchumi wetu’ anatarajiwa kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi.

spot_img

Latest articles

FCC yawahamasisha wananchi kulinda Afya na Haki zao dhidi ya Bidhaa Bandia

Na Tatu Mohamed TUME ya Ushindani (FCC) imewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kulinda...

PSPTB yatangaza Mitihani ya 31 ya Kitaaluma, Usajili kufungwa Agosti 15, mwaka huu

Na Tatu Mohamed BODI ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza kuendesha Mitihani ya...

Ewura CCC: Wananchi wadai fidia wanapocheleweshewa kuunganishiwa maji kwa siku saba za kazi

Na Tatu Mohamed BARAZA la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji...

Ridhiwani aipa tano Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na...

More like this

FCC yawahamasisha wananchi kulinda Afya na Haki zao dhidi ya Bidhaa Bandia

Na Tatu Mohamed TUME ya Ushindani (FCC) imewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kulinda...

PSPTB yatangaza Mitihani ya 31 ya Kitaaluma, Usajili kufungwa Agosti 15, mwaka huu

Na Tatu Mohamed BODI ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imetangaza kuendesha Mitihani ya...

Ewura CCC: Wananchi wadai fidia wanapocheleweshewa kuunganishiwa maji kwa siku saba za kazi

Na Tatu Mohamed BARAZA la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji...