Serikali yatambua mchango wa Kibanda katika tasnia ya habari, yampa zawadi

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Mwandishi wa Habari Mkongwe,  Absalom Kibanda ambaye pia ni Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Media Brains,  amezawadiwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutokana na mchango wake katika tasnia ya habari nchini.

Zawadi hiyo ya fedha taslimu Sh 10 milioni, imekabidhiwa jana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa utoaji tuzo za Samia  Kalamu  Awards 2025, jijini Dar es Salaam.

Kibanda amepewa zawadi hiyo pamoja na wakongwe wengine ambao ni Deodatus Balile, Haula Shamte na Baraka Islam  kutokana na uandishi wao mahiri wa habari na uchambuzi hasa katika masuala ya siasa.

Akizungumza wakati wa kutoa zawadi hizo, Prof. Kabudi amesema habari na makala ambazo wameziandika wakongwe  hao zimekuwa mchango mkubwa na zimewaleta watanzania pamoja bila kuligawa Taifa.

“Mheshimiwa Rais nawiwa wingi wa shukrani kwa  waandishi wenzangu wa habari, na wapo  waandishi wa habari mahiri wa habari za siasa zenye uchambuzi wa kina, zinazojenga umoja, uzalendo, mshikamano na zinazotambua hatua kubwa za kimaendeleo ambayo Taifa letu limepga hasa katika miaka hii minne ya uongozi wako.

“Habari na makala ambazo wameziandika Mheshimiwa Rais ni makala ambazo zimetuleta pamoja, zimetujenga pamoja na ni makala ambazo haziligawi Taifa. Kawa kutambua mchango wa hao waandishi wa habari, Wizara imeona ni vyema nao watunukiwe zawadi na wizara,” ameeleza Prof. Kabudi.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...

More like this

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...