Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Wawekezaji wakumbushwa kuendelea kuchangia katika miradi ya maendeleo

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu), Jenista Mhagam, ametoa rai kwa wawekezaji wa mbalimbali katika jimbo la Peramiho kuendelea Kufanya uwekezaji wenye tija kwa wananchi, kwa Halmashauri na kwa Taifa.

Waziri Mhagama ametoa rai hiyo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Muhukuru katika ziara yake ya kutembelea Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Songea Julai 12, 2023.

“Tunataka wawekezaji wajue wana wajibu wa kuchangia shughuli za maendeleo kwenye vijiji vinavozunguka maeneo uwekezaji,” amesisitiza.

Makaa ya mawe yamekuwa bidhaa muhimu na adhimu, uwekezaji umeendelea kukua na masoko yameongezeka, wawekezaji waangalie ajira zile zinazosaidia kuendesha miradi yao ili kutoa kipaombele katika maeneo ya vijjiji vilivyozunguka mradi, alisema Waziri Mhagama.

“Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi nzuri ya kuvutia Wawekezaji Mbalimbali, Wawekezaji wa shamba la miwa, wawekezaji wa makaa ya mawe na wawekezaji wa umeme wa maji, naomba kila Mwekezaji aliyeomba ardhi ya uwekezaji atumie kama alivyoomba,” amesema Mhagama.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea, Menas Komba amesema uwekezaji wa makaa ya mawe kuna mpango kabambe ambao umelenga kupata asilimia moja ya kila awamu ya mauzo.

“Tuendele kushirikiana na wawekezaji wanaokuja kuwekeza ili waendelee kutusaidia na Halmashauri itasimamia kupata haki za wananchi,” amesema Komba

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Songea, Mwalimu Neema Maghembe amesema wawekezaji wote waliowekeza katika Halmashauri ya Songea wamefuata taratibu zote za uwekezaji.

“Tunawawekezaji wa kutosha, wengine wanaendelea na kazi za tafiti mbalimbali na wengine wako katika hatua ya kuanza uchimbaji wa makaa ya mawe,” amesema Mwalimu Maghembe.

spot_img

Latest articles

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...

Wachina wanne wakamatwa kwa utekaji

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia raia wanne...

Watu 1,066 wapoteza maisha ajali za barabarani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Patrobas Katambi amesema jumla ya Watu 1,066...

Maombi ya Lissu kusikilizwa Juni 2, arudishwa rumande

Na Mwandishi Wetu MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masijala Ndogo ya Dar es Salaam, imepanga kusilikiza...

More like this

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...

Wachina wanne wakamatwa kwa utekaji

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia raia wanne...

Watu 1,066 wapoteza maisha ajali za barabarani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Patrobas Katambi amesema jumla ya Watu 1,066...