Majaliwa: Huduma Jumuishi za kifedha ni kiungo muhimu cha ukuaji uchumi

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa huduma jumuishi za kifedha ni kiungo muhimu cha ukuaji wa uchumi, kupunguza umaskini na kuchochea maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Amesema Serikali kwa kutambua hilo imedhamiria kuendelea kushirikiana na wadau wote ili kuhakikisha sekta ya kifedha inazidi kuwa jumuishi, fanisi, na yenye tija kwa maendeleo ya Taifa.

Amesema hayo leo Machi 3, 2025 alipozindua huduma mpya za kidijitali za Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) katika ukumbi wa Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam.

Ameongeza kuwa katika vipindi tofauti, Serikali imekuwa ikiandaa na kutekeleza mikakati ya Taifa ya kuboresha huduma jumuishi za kifedha.

“Mpango Mkakati wa Taifa wa Huduma Jumuishi za Fedha wa 2023 – 2028 ni mwendelezo wa mafanikio yaliyopatikana kupitia Mpango Mkakati wa Taifa wa Huduma Jumuishi za Fedha uliokamilika Desemba 2022,” amesema.

Majaliwa ameongeza kuwa jitihada nyingine ni kuandaa Mkakati wa Uchumi wa Kidijitali wa miaka 10 kuanzia mwaka 2024 hadi 2034.

“Mkakati huu umeainisha malengo mahsusi ambayo kama nchi tunaazimia kuyatekeleza ili kufikia uchumi wa kidijitali,” amesema Majaliwa.

Kwa upande wake, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Sauda Msemo amesema sekta ya fedha imeendelea kuwa na ustahimilivu na hivyo kuwezesha shughuli mbalimbali za kiuchumi kufanyika.

Aidha, Naibu Gavana huyo ametoa wito kwa taasisi zote za kifedha zifuate viwango bora vya usalama wa mitandao na kugundua haraka pale panapotokea udanganyifu wa aina yoyote.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi amesema lengo la uzinduzi wa huduma hizo za NBC kidijitali ni kuboresha utoaji wa huduma za kifedha na kuzifanya zipatikane kwa urahisi.

“Huduma hizo ni pamoja na ufunguaji wa akaunti, kuhamisha fedha, kupata mikopo bila ya kwenda katika tawi,”.

spot_img

Latest articles

Makamu wa Rais atangaza kujiuzulu

Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kuanzia...

RAIS SAMIA AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUJIANDAA NA UDHIBITI WA ATHARI ZA ELNINO

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

JNHPP kuongeza Umeme wa Gridi ya Taifa kwa asilimia 45

Na Tatu Mohamed BWAWA la Julius Nyerere (JNHPP) linatarajiwa kuongeza kwa kiasi kikubwa uwezo...

More like this

Makamu wa Rais atangaza kujiuzulu

Makamu wa Rais wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kuanzia...

RAIS SAMIA AAGIZA WAKUU WA MIKOA KUJIANDAA NA UDHIBITI WA ATHARI ZA ELNINO

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...

Rais Samia azindua Kituo cha kuzalisha Umeme cha Julius Nyerere

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan,...