RAIS MWINYI:TUSIPANDISHE BEI ZA BIDHAA ZA VYAKULA WAKATI WA RAMADHANI

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuridhishwa na upatikanaji wa bidhaa za vyakula na kuwataka wafanyabiashara kutopandisha bei wakati Ramadhani itakapoanza.

Rais Dk.Mwinyi amesema hayo alipotembelea Masoko ya Jumbi, Mwanakwerekwe na Darajani kuangalia mwenendo wa biashara na upatikanaji wa bidhaa za vyakula kuelekea mwezi wa Ramadhani.

Ameeleza kuwa Serikali inajipanga kwa ajili ya Ujenzi wa Masoko mengine maeneo mbalimbali ili kila mfanyabiashara afanye biashara kwenye mazingira rasmi .

Kuhusu usafi wa masoko ameuagiza uongozi wa masoko hayo kutafuta njia bora zaidi ya uhifadhi wa bidhaa za wafanyabiashara ili masoko kuwa safi wakati wote.

Amezielekeza taasisi zinazosimamia masoko hayo kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya maji na vipooza hewa katika masoko yote pamoja na kuimarisha usafi.

Ziara hiyo ya Rais Mwinyi ni ya kwanza tangu kufunguliwa kwa masoko mapya ya Jumbi , Mwanakwerekwe na ukarabati mkubwa wa Soko la Darajani.

spot_img

Latest articles

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

More like this

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...