Rais Samia kufanya ziara nchini Ethiopia, kushiriki Mkutano wa Au

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kufanya ziara ya kikazi Addis Ababa nchini Ethiopia kuanzia leo Februari 14 hadi 16 kushiriki mkutano wa kawaida wa 38 wa Nchi na serikali wa Umoja wa Afrika (AU).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Sharifa Nyanga, imeeleza kuwa mkutano huo unatarajia kuchagua mwenyekiti mpya wa AU kwa mwaka 2025 atakayechukua nafasi ya mwenyekiti wa sasa Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania.

Pia, mkutano huo pia utachagua viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ikiwemo mwenyekiti, makamu mwenyekiti na makamishna sita.

“Aidha, mkutano huo pia utachagua viongozi wapya wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika ikiwemo Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Makamishna 6.

“Vilevile, Mkutano utajadili Taarifa ya Ushiriki wa Umoja wa Afrika kwenye Mkutano wa Nchi Tajiri Duniani (G20), Utekelezaji wa Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika na Taarifa kuhusu masuala ya mabadiliko ya tabianchi,” imeeleza taarifa hiyo.

Imeongeza kuwa mbali na masuala hayo, Mkutano utajadili Ajenda kuhusu Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia iliyopendekezwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Kabla ya kushiriki Mkutano wa 38, Rais Dkt. Samia atashiriki Mkutano wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika utakaofanyika Februari 14,

spot_img

Latest articles

DC Kibaha afungua Baraza Kuu la Wafanyakazi DAWASA

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Simon amefungua kikao cha Baraza...

Lukuvi aitaka Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuweka mifumo rafiki ya usambazaji nyaraka kwa Wananchi

Na Mwandishi Wetu IDARA Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali yatakiwa kuweka mifumo mizuri ya...

Mramba: Umeme wa Jotoardhi kuunganishwa kwenye gridi ya Taifa ifikapo 2030

📌 *Mikoa 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi 📌 SEforALL yatakiwa kuwekeza katika...

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Dharura wa SADC kwa njia ya mtandao

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya...

More like this

DC Kibaha afungua Baraza Kuu la Wafanyakazi DAWASA

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Simon amefungua kikao cha Baraza...

Lukuvi aitaka Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuweka mifumo rafiki ya usambazaji nyaraka kwa Wananchi

Na Mwandishi Wetu IDARA Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali yatakiwa kuweka mifumo mizuri ya...

Mramba: Umeme wa Jotoardhi kuunganishwa kwenye gridi ya Taifa ifikapo 2030

📌 *Mikoa 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi 📌 SEforALL yatakiwa kuwekeza katika...