AJALI YAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA, DODOMA JIJI

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeahirisha   mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara  kati ya  Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kuchezwa  Februari 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi hiyo, kuahirisha mchezo huo kumetokana na hali ya kiafya ya maofisa na wachezaji wa Dodoma Jiji kutokuwa nzuri baada ya ajali ya basi waliyopata wakati wakisafiri kutokea Ruangwa mkoani Lindi.

“Ajali hiyo imesababisha athari hasi kwa klabu ya Dodoma Jiji kwa kuchelewesha safari yake ya kuelekea mkoani Dar es Salaam pamoja na kuathiri maandalizi ya kiufundi kwa kuwakosa wachezaji na maofisa wa ufundi ambao walipata majeraha katika ajali hiyo. Bodi itatangaza tarehe mpya ya mchezo huo hivi karibuni,” imesema taarifa hiyo.

Aidha kwa upande wa taarifa ya klabu ya Dodoma Jiji, kikosi hicho kimewasili salama jijini Dodoma na  ambapo taratibu za kitabibu zitaendelea kwa majeruhi wote katika Hosptali ya Benjamin Mkapa. 

Dodoma Jiji ilipata ajali Februari 10, 2025 baada ya basi walikuwa wakisafiria kutumbukia mtoni katikati ya Nangurukuru na Somanga.

spot_img

Latest articles

DC Kibaha afungua Baraza Kuu la Wafanyakazi DAWASA

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Simon amefungua kikao cha Baraza...

Lukuvi aitaka Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuweka mifumo rafiki ya usambazaji nyaraka kwa Wananchi

Na Mwandishi Wetu IDARA Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali yatakiwa kuweka mifumo mizuri ya...

Mramba: Umeme wa Jotoardhi kuunganishwa kwenye gridi ya Taifa ifikapo 2030

📌 *Mikoa 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi 📌 SEforALL yatakiwa kuwekeza katika...

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Dharura wa SADC kwa njia ya mtandao

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya...

More like this

DC Kibaha afungua Baraza Kuu la Wafanyakazi DAWASA

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Simon amefungua kikao cha Baraza...

Lukuvi aitaka Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuweka mifumo rafiki ya usambazaji nyaraka kwa Wananchi

Na Mwandishi Wetu IDARA Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali yatakiwa kuweka mifumo mizuri ya...

Mramba: Umeme wa Jotoardhi kuunganishwa kwenye gridi ya Taifa ifikapo 2030

📌 *Mikoa 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi 📌 SEforALL yatakiwa kuwekeza katika...