AJALI YAAHIRISHA MCHEZO WA SIMBA, DODOMA JIJI

Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeahirisha   mchezo Ligi Kuu Tanzania Bara  kati ya  Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kuchezwa  Februari 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi hiyo, kuahirisha mchezo huo kumetokana na hali ya kiafya ya maofisa na wachezaji wa Dodoma Jiji kutokuwa nzuri baada ya ajali ya basi waliyopata wakati wakisafiri kutokea Ruangwa mkoani Lindi.

“Ajali hiyo imesababisha athari hasi kwa klabu ya Dodoma Jiji kwa kuchelewesha safari yake ya kuelekea mkoani Dar es Salaam pamoja na kuathiri maandalizi ya kiufundi kwa kuwakosa wachezaji na maofisa wa ufundi ambao walipata majeraha katika ajali hiyo. Bodi itatangaza tarehe mpya ya mchezo huo hivi karibuni,” imesema taarifa hiyo.

Aidha kwa upande wa taarifa ya klabu ya Dodoma Jiji, kikosi hicho kimewasili salama jijini Dodoma na  ambapo taratibu za kitabibu zitaendelea kwa majeruhi wote katika Hosptali ya Benjamin Mkapa. 

Dodoma Jiji ilipata ajali Februari 10, 2025 baada ya basi walikuwa wakisafiria kutumbukia mtoni katikati ya Nangurukuru na Somanga.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...