TANZANIA NA URUSI ZAIMARISHA USHIRIKIANO WA UTALII KUPITIA MAKUBALIANO MAPYA

Na Mwandishi Wetu

TANZANIA na Urusi zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya utalii, hatua inayolenga kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili na kuongeza fursa za utalii, biashara na uwekezaji.

Makubaliano hayo yanaenda sambamba na kuanza kwa safari za moja kwa moja za kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) zinazounganisha Moscow na Tanzania Bara pamoja na Zanzibar, hatua itakayorahisisha usafiri wa watalii na wafanyabiashara kati ya masoko hayo mawili.

Katika safari hiyo ya kihistoria ya kwanza, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji, aliongoza ujumbe wa Tanzania uliojumuisha Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na wadau zaidi ya kampuni 47 za utalii.Ujumbe huo ulikutana na wadau wa sekta ya utalii kutoka Urusi kupitia mikutano ya biashara baina ya wafanyabiashara (B2B), iliyowapa fursa ya kujadiliana, kujenga ushirikiano mpya wa kibiashara na kutangaza vivutio vya kipekee vya utalii vya Tanzania kwa soko la Urusi.

Hatua hii inatarajiwa kuongeza idadi ya watalii kutoka Urusi, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika sekta ya utalii, na kuchangia utekelezaji wa malengo ya Tanzania ya kukuza sekta ya utalii na uchumi wa nchi kupitia masoko mapya ya kimkakati.

spot_img

Latest articles

Mhitimu wa VETA abuni mashine za kuongeza thamani ya mazao, ajiajiri kupitia kampuni yake

Na Mwandishi Wetu MHITIMU wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia VETA, Ernest Maranya, amebuni...

MHE.SALOME: WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000

Na Mwandishi Wetu, Mara Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu...

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...

Ofisi ya Usuluhishi wa Kodi Yaahidi Kuimarisha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi imesema, inaendelea...

More like this

Mhitimu wa VETA abuni mashine za kuongeza thamani ya mazao, ajiajiri kupitia kampuni yake

Na Mwandishi Wetu MHITIMU wa mafunzo ya ufundi stadi kupitia VETA, Ernest Maranya, amebuni...

MHE.SALOME: WANANCHI WANAOPITIWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME WAUNGANISHIWE HUDUMA KWA SH. 27,000

Na Mwandishi Wetu, Mara Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amesema Serikali ya Awamu...

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...