Wanajeshi 75 wapandishwa kizimbani kwa kukimbia mapigano na M23

Na Mwandishi Wetu

Wanajeshi 75 wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) wanapandishwa kizimbani leo Februari 10, 2025 wakituhumiwa kukimbia mapigano baina ya vikosi vya Serikali na waasi wa M23.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka ya Kijeshi wa DRC imeeleza kuwa askari hao pia wanashtakiwa kwa tuhuma za kufanya vurugu dhidi ya raia ikiwa ni pamoja na mauaji na uporaji.

“Wanajeshi 75 wanaokabiliwa na kesi walikamatwa kwa kukimbia mapigano baada ya kushikiliwa kwa Mji wa Nyabibwe. Wanatuhumiwa kwa ubakaji, mauaji, uporaji na uasi,”. imeeleza taarifa hiyo.

Umoja wa Mataifa umeripoti kuwepo kwa vitendo kadhaa vikiwemo ya unyongaji, ubakaji wa magenge na utumwa wa kingono hasa katika eneo la Mashariki la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imedai kuwa waasi wa M23 na askari wa Serikali ya DRC pamoja na wanamgambo wanaoiunga mkono Serikali wote wanahusika.

spot_img

Latest articles

FADLU ATAKA USHINDI WA MABAO 4 KWA AL MASRY

Na Mwandishi Wetu Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema katika mchezo wa kesho wa...

Kiungo fundi Yanga kuikosa Azam

Na Mwandishi Wetu Kiungo wa Yanga Khalid Aucho atakosekana katika mchezo  wa Ligi Kuu Bara...

Kada wa Chadema amuomba msajili wa vyama vya siasa kubatilisha Baraza Kuu la chama hicho lililoketi Januari 22, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Mwanga,...

GSM, EFTA zaungana kuwabeba wafanyabiashara wadogo na kati

Na Mwandishi Wetu Taasisi ya kifedha ya EFTA na GSM zimeungana kwa kusaini mkataba wa...

More like this

FADLU ATAKA USHINDI WA MABAO 4 KWA AL MASRY

Na Mwandishi Wetu Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema katika mchezo wa kesho wa...

Kiungo fundi Yanga kuikosa Azam

Na Mwandishi Wetu Kiungo wa Yanga Khalid Aucho atakosekana katika mchezo  wa Ligi Kuu Bara...

Kada wa Chadema amuomba msajili wa vyama vya siasa kubatilisha Baraza Kuu la chama hicho lililoketi Januari 22, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Mwanga,...