Ramovic awaita mashabiki uwanjani, anapenda kuitwa Tanzanian Machine

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa Yanga,Sead Ramovic amesema mashabiki wanamuita ‘German Machine’ lakini yeye angependa kuitwa ‘Tanzanian Machine’, huku akiwaita mashabiki wa timu hiyo kesho kujitokeza uwanjani ili kukaribisha na kumsapoti ili kupata matokeo mazuri.

Yanga kesho Novemba 26,2024 inashuka dimbani kucheza na Al Hilal katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika  kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.  

“Mashabiki wananiita German Machine, lakini mimi ukiniuliza ningependa kuitwa Tanzanian Machine, nataka kufurahi pamoja na watu wa hapa na kuhakikisha klabu hii inapata mafanikio,” amesema Ramovic.

Aidha amesema Yanga ni timu bora lakini pia wanakwenda kucheza na timu bora, hivyo wanahitaji umakini kukabiliana na mchezo huo mgumu.

“Hii ni mara yangu ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa. Ni jambo la kheri sana kwangu kushiriki mashindano haya makubwa nikiwa na timu kubwa. Falsafa yangu kubwa ni nidhamu na kujituma. Napenda kuona wachezaji wakicheza kama timu, haijalishi unatumia mfumo gani kama wachezaji wako hawana umoja ni ngumu kupata matokeo,” ameeleza.

Kocha huyo amesema katika timu yao hakuna mtu ambaye ni staa kwa sababu kila mtu ni staa ndani ya kikosi hicho.

Kwa upande wake nahodha wa timu hiyo Bakari Mwamnyeto amesema anajua kwamba mechi ya kesho itakuwa ngumu lakini wapinzani wao wajipange kwani wasipoangalia wanaweza kula hata goli tano.

spot_img

Latest articles

Sakata lake na Harmonize, Ibraah aiachia Basata

Na Mwandishi Wetu Baada ya kutoka ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), msanii...

Waziri Mkuu ashiriki ufunguzi wa jukwaa la maafisa watendaji wakuu Afrika 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameshiriki ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili...

TFF kuja mshirika wa kubashiri mechi zake

Na Mwandishi Wetu Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika...

Viongozi mbalimbali washiriki ibada ya kuaga mwili wa Cleopa Msuya

Viongozi mbalimbali wa Serikali na wananchi wakiaga mwili wa aliyekuwa Makamu wa kwanza wa...

More like this

Sakata lake na Harmonize, Ibraah aiachia Basata

Na Mwandishi Wetu Baada ya kutoka ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), msanii...

Waziri Mkuu ashiriki ufunguzi wa jukwaa la maafisa watendaji wakuu Afrika 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameshiriki ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili...

TFF kuja mshirika wa kubashiri mechi zake

Na Mwandishi Wetu Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika...