Watu wawili wafariki, 16 wajeruhiwa katika ajali ya basi Songwe

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Watu wawili wamefariki dunia na wengine 16 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugonga daraja na kutumbukia mtoni katika eneo la Mlima Myovizi, mkoani Songwe.

Ajali hiyo, iliyotokea leo Julai 15 saa 12 asubuhi, ilihusisha basi la Ngasere High Class lililokuwa likisafiri kutoka Dodoma kwenda Tunduma, mkoani Songwe.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, Gallus Hyera, amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo viwili na majeruhi 16 katika ajali hiyo, ambayo ilitokea baada ya basi hilo kugonga nguzo ya daraja na kutumbukia mtoni.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, Dk. Kelvin Masae, amethibitisha kupokea majeruhi 16 ambao wanaendelea kupatiwa matibabu, huku wengine wakipewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...