VAR kutumika ligi kuu bara msimu ujao

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Ili kupunguza makosa ya waamuzi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara Serikali imependekeza kutumika kwa Teknolojia ya Kuwasaidia Waamuzi (VAR) kuanzia msimu ujao huku ikitoa msamaha wa kodi kwenye uingizaji wa mashine hizo.

Mapendekezo hayo yametangazwa Juni 13,2024 Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, wakati akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Amesema VAR itasaidia kuleta ufanisi na kuhakikisha matokeo yanayopatikana uwanjani yanakuwa ya haki.

“Kuna timu msimu mmoja penati 10 halafu zikifungwa zenyewe magoli yanakataliwa, na ili tuwe na VAR za kutosha naleta penndekezo la kutoa msamaha kwenye uingizaji wa mashine za VAR na vifaa vyake,” amesema Dk. Nchemba.

spot_img

Latest articles

Mufti Zubeir asisitiza upendo, kupuuza wanaoneza chuki za kidini mtandaoni

Na Mwandishi Wetu MUFTI na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally ametoa...

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

More like this

Mufti Zubeir asisitiza upendo, kupuuza wanaoneza chuki za kidini mtandaoni

Na Mwandishi Wetu MUFTI na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally ametoa...

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...