Mtu mmoja afariki katika ajali ya ndege ya shirika la ndege la Singapore kutoka London

Bangkok, Thailand

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa leo wakati ndege ya shirika la ndege la Singapore kutoka London Uingereza kuekea Singapore ilipokumbwa na msukosuko mkubwa, shirika hilo la ndege limethibitisha.

Ndege hiyo aina ya Boeing 777-300ER ilielekezwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi huko Bangkok, Thailand, ambako ilitua kwa dharura saa 3:45pm (08:45 GMT) leo Jumanne.

Ndege ya SQ321 “ilikumbana na msukosuko mkubwa njiani,” Shirika la Ndege la Singapore limeeleza katika taarifa kwenye ukurasa wake wa Facebook.

“Tunaweza kuthibitisha kuwa kuna majeruhi na mtu mmoja aliyefariki kwenye ndege ya Boeing 777-300ER,” ilisema.

Saa nne baada ya kutua kwa dharura, watu 18 walisalia hospitalini huku wengine 12 wakitibiwa kwa msingi wa wagonjwa wa nje, imeeleza taarifa hiyo.

“Abiria na wafanyakazi waliosalia wanachunguzwa na kupewa matibabu, inapobidi,” iliongeza.

Ndege hiyo ilikuwa na abiria 211 na wahudumu 18.

Kittipong Kittikachorn, meneja mkuu wa Uwanja wa ndege wa Suvarnabhumi, aliambia mkutano wa wanahabari kwamba mwathiriwa alikuwa Muingereza ambaye alionekana kuwa na mshtuko wa moyo.

Kundi la Viwanja vya Ndege vya Thailand lilisema abiria waliojeruhiwa kidogo na ambao hawajajeruhiwa wanasaidiwa katika eneo maalum lililowekwa ndani ya kituo kwenye Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi.

spot_img

Latest articles

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

More like this

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...