Uokoaji waendelea kutafuta watu 20 walioporomoka na daraja la Francis Scott Key Marekani

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Timu za kutafuta na kuokoa zinawatafuta karibu watu 20 ambao hawajulikani walipoa baada ya daraja kubwa kuporomoka katika mji wa Baltimore, Maryland Marekani.

Video ya simu ilionyesha sehemu kadhaa za daraja hilo la Francis Scott Key likianguka kwenye Mto Patapsco baada ya meli ya kontena yenye bendera ya Singapore inayoitwa Dali kugonga nguzo ya Daraja hilo Jumanne alfajiri.

Maafisa wa usalama waasema magari kadhaa yalikuwa kwenye daraja wakati ajali hiyo ilipotokea.

Maafisa wa dharura wa Baltimore wanasema wafanyakazi wa utafutaji na uokoaji wanatafuta takriban watu 20 wanaoaminika kuwa ndani ya maji.

Wasimamizi wa meli ya Dali, Synergy Marine Corp, walitoa taarifa wakisema kuwa meli hiyo iligonga nguzo moja ya daraja hilo na kwamba wafanyakazi wake wote wakiwemo manahodha wawili waliokuwemo wamepatikana na hakuna taarifa zozote za majeruhi

spot_img

Latest articles

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...