Polisi wawasaka walioua, kukata nyeti za marehemu

Polisi mkoani Mwanza wanawasaka wahusika wa mauaji ya Masanja Kefa (32) mkazi wa Kijiji cha Mwagig’hi, Kata ya Nkalalo wilayani kwimba, kukata sehemu zake za siri kisha kutoweka nazo. Tukio hilo linalohusishwa na imani za ushirikina, Februari 12, 2024.

Ofisa Polisi Jamii Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhani Sarige amesema wakati polisi wakiedelea na uchunguzi wa tukio hilo, wakazi wa Kijiji cha Mwagig’hi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa ambazo zitawezesha waliotenda uhalifu huo kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

ACP Sarige amesema hayo Februari 26, 2024 akiwa ameambatana na baadhi ya maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali wakati wakitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wakazi wa kijiji hicho.

“Tumewaletea Polisi Kata lengo likiwa ni kuimarisha ulinzi shirikishi lakini mmempokea kwa tukio hili la kikatili, si vyema kuendekeza vitendo hivi vya kishirikiana, tuhakikishe tunashirikiana katika ulinzi shirikishi ili kukomesha vitendo hivi,”anasema Sarige na kuongeza:

“Tunajua watu hawa mnawafahamu na wengine wanaweza kuwa ni ndugu zetu, hivyo tusiwafiche wahalifu hawa kwani leo kwake, kesho kwako. Kama kafanya hivyo kwa huyo, umemtunza kesho atakufanyia wewe.”

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamewapongeza polisi kwa kuimarisha ushirikiano na kuwa karibu hasa wakati huu ambao wamesema ni mgumu, na wameahidi kutoa ushirikiano ili kuwapata wahalifu waliohusika na tukio.

spot_img

Latest articles

Mhudumu wa mochwari mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na viungo vya binadamu

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu wawili akiwamo mhudumu wa mochwari...

Katibu wa fedha UVCCM Dar arudisha fomu ya ridhaa ya ubunge Kawe

Katibu wa Uchumi, Mipango na Fedha UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Hassan Ali...

Majaliwa  atangaza hagombei tena ubunge Ruangwa

Na Mwandishi Wetu Waziri mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa leo Julai...

Vijana, Dira na CCM. Chama pekee chenye Imani na vijanaTangu kuasisiwa

Na Mwandishi Wetu TANGU kuasisiwa kwake tarehe 5 Februari 1977 kwa muungano wa TANU...

More like this

Mhudumu wa mochwari mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na viungo vya binadamu

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu wawili akiwamo mhudumu wa mochwari...

Katibu wa fedha UVCCM Dar arudisha fomu ya ridhaa ya ubunge Kawe

Katibu wa Uchumi, Mipango na Fedha UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Hassan Ali...

Majaliwa  atangaza hagombei tena ubunge Ruangwa

Na Mwandishi Wetu Waziri mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa leo Julai...