Polisi wawasaka walioua, kukata nyeti za marehemu

Polisi mkoani Mwanza wanawasaka wahusika wa mauaji ya Masanja Kefa (32) mkazi wa Kijiji cha Mwagig’hi, Kata ya Nkalalo wilayani kwimba, kukata sehemu zake za siri kisha kutoweka nazo. Tukio hilo linalohusishwa na imani za ushirikina, Februari 12, 2024.

Ofisa Polisi Jamii Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhani Sarige amesema wakati polisi wakiedelea na uchunguzi wa tukio hilo, wakazi wa Kijiji cha Mwagig’hi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa ambazo zitawezesha waliotenda uhalifu huo kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

ACP Sarige amesema hayo Februari 26, 2024 akiwa ameambatana na baadhi ya maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali wakati wakitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wakazi wa kijiji hicho.

“Tumewaletea Polisi Kata lengo likiwa ni kuimarisha ulinzi shirikishi lakini mmempokea kwa tukio hili la kikatili, si vyema kuendekeza vitendo hivi vya kishirikiana, tuhakikishe tunashirikiana katika ulinzi shirikishi ili kukomesha vitendo hivi,”anasema Sarige na kuongeza:

“Tunajua watu hawa mnawafahamu na wengine wanaweza kuwa ni ndugu zetu, hivyo tusiwafiche wahalifu hawa kwani leo kwake, kesho kwako. Kama kafanya hivyo kwa huyo, umemtunza kesho atakufanyia wewe.”

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamewapongeza polisi kwa kuimarisha ushirikiano na kuwa karibu hasa wakati huu ambao wamesema ni mgumu, na wameahidi kutoa ushirikiano ili kuwapata wahalifu waliohusika na tukio.

spot_img

Latest articles

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

More like this

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...