EWURA: Ukaguzi wa mifumo ya umeme kila baada ya miaka mitano unaweza kuzuia majanga ya moto

Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imewataka wananchi kujenga utamaduni wa kukagua mifumo ya umeme majumbani kila baada ya miaka mitano, ikisema hatua hiyo inaweza kubaini mapema hitilafu zinazoweza kusababisha moto, uharibifu wa mali na hata kupoteza maisha.

Akizungumza katika Maonesho ya Kitaifa ya Wakulima ‘Nanenane’ yanayoendelea jijini Dodoma, Meneja wa EWURA Kanda ya Kati, Hawa Lweno, amesema wananchi wengi huamini mfumo wa umeme hubaki salama baada ya kufungwa, jambo ambalo si sahihi.

“Kupata cheti cha usalama wakati mfumo wa umeme unapofungwa haimaanishi kuwa utakuwa salama maisha yote. Tunashauri mfumo ukaguliwe tena kila baada ya miaka mitano na fundi mwenye leseni ili kubaini mapema hitilafu zinazoweza kusababisha moto,” amesema.

Amebainisha kuwa, nyaya zilizochakaa, vifaa vilivyoharibika au mabadiliko ya matumizi ya umeme ndani ya nyumba ni baadhi ya sababu zinazoweza kuongeza hatari ya moto ikiwa ukaguzi wa mara kwa mara hautafanyika.

Mbali na umeme, EWURA pia imewataka wananchi kuzingatia matumizi salama ya gesi ya kupikia (LPG) kwa kuhakikisha mitungi inawekwa sehemu zenye hewa ya kutosha na vifaa vyake, ikiwemo regulator na jiko, vinakuwa katika hali nzuri.

“Baada ya kutumia gesi hakikisha unazima jiko na regulator. Pia ni muhimu kila anayehusika na matumizi ya gesi nyumbani apewe elimu ya matumizi salama ili kupunguza ajali zinazoweza kuepukika,” amesema.

Ameongeza kuwa mtungi mpya wa gesi unapaswa kuachwa kwa dakika 15 hadi 20 kabla ya kuanza kutumika ili kuruhusu gesi kutulia na kuongeza usalama wakati wa matumizi.

Katika sekta ya maji, Lweno amewataka wananchi kukagua mara kwa mara mabomba ya ndani ya nyumba ili kubaini uvujaji wa maji unaoweza kuongeza matumizi na bili zisizo za lazima.

“Kabla ya kudhani bili imeongezeka kutokana na kosa la usomaji wa mita, kwanza hakikisha hakuna uvujaji wa maji katika mfumo wa mabomba ya nyumba yako. Pia fuatilia usomaji wa mita kila unapofanyika,” amesema.

Amesema EWURA inaendelea kutumia Maonesho ya Nanenane kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya huduma za umeme, gesi na maji pamoja na haki na wajibu wa watumiaji wa huduma hizo.

Kwa mujibu wa Lweno, wananchi wameendelea kujitokeza kwa wingi kutembelea banda la EWURA, ambapo zaidi ya watu 600 walikuwa wamepata elimu kuhusu usalama wa matumizi ya nishati na maji tangu kuanza kwa maonesho hayo.

Amewahimiza wananchi kuendelea kutafuta elimu kutoka EWURA ili kuongeza usalama wa familia zao, kulinda mali na kuhakikisha matumizi bora ya huduma za nishati na maji.

spot_img

Latest articles

UDOM yabuni mfumo wa kidijitali wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaowezesha wakulima kufuatilia...

ZSTC yapongeza mchango wa TADB katika kukuza sekta ya karafuu Zanzibar

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) limesema ushirikiano wake na...

Mikopo ya TADB yaongeza nguvu biashara ya parachichi, Eatfresh yawahakikishia wakulima soko

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Eatfresh (GBRI Business Solutions) imesema ufadhili wa zaidi ya Sh...

GST: Tafiti za Jiosayansi ni Nguzo ya Dira ya Taifa 2050 na Uchumi Endelevu wa Madini

Na Mwandishi Wetu, Dodoma MWENYEKITI wa Bodi ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini...

More like this

UDOM yabuni mfumo wa kidijitali wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaowezesha wakulima kufuatilia...

ZSTC yapongeza mchango wa TADB katika kukuza sekta ya karafuu Zanzibar

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) limesema ushirikiano wake na...

Mikopo ya TADB yaongeza nguvu biashara ya parachichi, Eatfresh yawahakikishia wakulima soko

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI ya Eatfresh (GBRI Business Solutions) imesema ufadhili wa zaidi ya Sh...