WANANCHI WAHAMASISHWA KUTUMIA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI ILI KUPUNGUZA GHARAMA ZA USAFIRI

📌 TANESCO yaeleza matumizi ya umeme katika magari, bajaji na pikipiki

📌 Pikipiki ya umeme hutumia uniti 3 pekee kusafiri hadi kilometa 130

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Wananchi wamehimizwa kutumia umeme katika vyombo vya usafiri ili kupunguza gharama za uendeshaji na kuchangia matumizi ya nishati safi na yenye ufanisi.

Akizungumza Julai 5, 2026 katika Banda la TANESCO kwenye Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Saba Saba), Afisa Uhusiano wa TANESCO, Bi. Amanda Tagame, amesema teknolojia ya usafiri wa kutumia umeme haipo kwenye magari pekee, bali pia inapatikana katika bajaji na pikipiki.

Ameeleza kuwa pikipiki ya umeme hutumia wastani wa uniti tatu za umeme zenye thamani ya takribani shilingi 1,500 na inaweza kusafiri hadi kilometa 130 kwa chaji moja, jambo linaloifanya kuwa chaguo la gharama nafuu na lenye ufanisi kwa watumiaji.

“Tunaposema endesha kwa umeme hatumaanishi katika magari pekee, bali pia katika bajaji na piki piki, ukitumia nishati ya umeme kwenye pikipiki ni nafuu sana ,hutumia wastani wa uniti 3 za umeme zenye thamani ya takribani shilingi 1,500, zinazowezesha kusafiri hadi kilometa 130”alifafanua Bi. Tagame.

Bi. Tagame amesema TANESCO itaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi ya umeme katika sekta ya usafiri ili kuwawezesha kufanya maamuzi yanayowanufaisha kiuchumi na kuunga mkono matumizi ya nishati safi.

spot_img

Latest articles

NACTVET yahamasisha elimu ya amali, yataka wazazi kuwapeleka watoto kwenye mafunzo ya ufundi

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi...

GCLA yatumia Sabasaba kutoa elimu ya usalama wa kemikali na huduma za maabara

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) imesema imejipanga kutumia...

TTB YAMKABIDHI KHALID AL BARWANI UBALOZI WA HIARI WA UTALII KUITANGAZA TANZANIA DUNIANI

Na Mwandishi Wetu BODI ya Utalii Tanzania (TTB) imemkabidhi rasmi mwanautalii na mtangazaji wa...

Serikali yaongeza msukumo wa kuwajengea vijana ujuzi unaokidhi soko la ajira

Na Mwandishi Wetu Serikali imesema itaendelea kuwekeza katika programu za kuwawezesha vijana kupata ujuzi...

More like this

NACTVET yahamasisha elimu ya amali, yataka wazazi kuwapeleka watoto kwenye mafunzo ya ufundi

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi...

GCLA yatumia Sabasaba kutoa elimu ya usalama wa kemikali na huduma za maabara

Na Mwandishi Wetu Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) imesema imejipanga kutumia...

TTB YAMKABIDHI KHALID AL BARWANI UBALOZI WA HIARI WA UTALII KUITANGAZA TANZANIA DUNIANI

Na Mwandishi Wetu BODI ya Utalii Tanzania (TTB) imemkabidhi rasmi mwanautalii na mtangazaji wa...