TPDC kuongeza uzalishaji wa gesi kupitia visima vipya

Na Mwandishi Wetu

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limesema linatarajia kuongeza uzalishaji wa gesi asilia nchini kupitia mradi wa uchorongaji wa visima vitatu katika Kitalu cha Mnazi Bay, ambapo visima viwili tayari vimekamilika na kimoja kinaendelea kuchorongwa.

Akizungumza katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), Mjiolojia wa TPDC, Magambo Samweli, alisema visima hivyo vinachimbwa kwa ubia kati ya TPDC na kampuni ya Maurel & Prom (M&P) kwa lengo la kuongeza kiwango cha gesi kinachozalishwa katika kitalu hicho.

Alisema kati ya visima vitatu vinavyochimbwa, viwili vinalenga kuongeza uzalishaji wa gesi, huku kisima kimoja kikitumika kutafuta maeneo mapya yenye akiba ya gesi asilia.


Kwa mujibu wa Samweli, kisima kimoja kina uwezo wa kuzalisha futi za ujazo milioni 40 za gesi kwa siku, huku kingine kikitarajiwa kuzalisha futi za ujazo milioni 60 kwa siku, hatua itakayoongeza upatikanaji wa gesi kwa matumizi mbalimbali nchini.

Mbali na mradi wa Mnazi Bay, TPDC kwa kushirikiana na kampuni ya ARA Petroleum inaendelea kuendeleza Kitalu cha Ruvuma, ambako tayari kumekuwa na ugunduzi mkubwa wa gesi katika eneo la Ntorya.

Alisema kwa sasa ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi kutoka visimani hadi Kituo cha Kuchakata Gesi cha Madimba unaendelea.

“Bomba hilo lenye urefu wa kilomita 34.2 na kipenyo cha inchi 14 litasafirisha gesi kutoka vitalu vya Ntorya na Ruvuma kwenda Madimba kwa ajili ya kusafishwa kabla ya kuingizwa kwenye bomba kuu la taifa linalopeleka gesi hadi Dar es Salaam,” alisema.

Samweli alisema ujenzi wa bomba hilo unatarajiwa kukamilika kati ya Novemba na Desemba mwaka huu, huku usafirishaji wa gesi kupitia bomba hilo ukitarajiwa kuanza mwezi Desemba 2026.

Alieleza kuwa kuanza kwa uzalishaji kutoka kwenye visima vipya kutaongeza kiwango cha gesi kinachoingia kwenye bomba kuu la taifa, hatua itakayosaidia kuongeza upatikanaji wa gesi kwa ajili ya uzalishaji wa umeme, matumizi ya viwandani, magari yanayotumia gesi pamoja na matumizi ya majumbani.

Alisema TPDC itaendelea kushirikiana na wawekezaji katika kuharakisha utafutaji na maendeleo ya rasilimali za gesi asilia ili kuhakikisha nchi inanufaika zaidi na nishati hiyo katika kukuza uchumi na maendeleo ya viwanda.

spot_img

Latest articles

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...

COASCO: Ukaguzi wa vyama vya ushirika waongeza uwazi na kuimarisha imani ya wanachama

Na Tatu Mohamed Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) limesema ukaguzi...

More like this

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

MAULIDI KITENGE AUNGANA NA TANESCO KUHAMASISHA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA UMEME

📌 Aahidi kutumia jukwaa lake kuhamasisha wananchi kutumia umeme kwa shughuli za kupikia 📌 Ushirikiano...