Na Winfrida Mtoi
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya beki wa zamani wa Manchester United, Rio Ferdinand nchini si kwa ajili ya ‘kuposti’ katika mitandao yake ya kijamii, bali kuona vipaji vya kitanzania kupitia taasisi yake na kusaidia kuvipaisha duniani.
Makonda ametoa kauli hiyo leo Mei 22, 2026 baada ya kuwepo kwa mijadala juu ya mchezaji huyo kutoposti ziara yake ya Tanzania katika mitandao yake ya kijamii.
Waziri huyo ameweka bayana kuwa ndiye alimuomba Rio asiposti chochote, kwani ndoto yake ilikuwa ni kumleta kusaidia vijana katika kuendeleza vipaji vyao kimataifa kwa sababu mchezaji huyo anajua kona zote za dunia.

“Agenda kubwa inayoendelea mjini hasa nchini ni Rio kuposti, kwa nini Rio hajaposti ni posti gani unataka Rio aposti pale? Tunapenda kujadili mambo kwa kuyaona bila kuyajua, tunaamini tunajua kila kitu.
“Ushawahi kufikiri mtu uko naye, anaongelea mema juu ya nchi yako, anaongelea juu ya serikali inayopiga hatua alafu wewe badala kuchukua ile posti uipeleke duniani unataka aposti yeye. Akiposti yeye ndio utajua yuko Tanzania?,”
Amesisitiza kuwa posti ni siku moja lakini akimtoa mtoto mmoja wa kitanzania ni mafanikio makubwa, hivyo Serikali itaendelea kushirikiana na watu wakubwa duniani kuitangaza Tanzania.


